Biblia ya mtandaoni

Matangazo

Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya


Zaburi 130 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Swahili Revised Union Version - SRUVDC
Zaburi 130

Kusubiri wokovu wa Mungu Wimbo wa kupanda mlima.

1 Ee BWANA, toka vilindini nimekulilia.

2 Bwana, uisikie sauti yangu. Masikio yako na yaisikilize Sauti ya dua zangu.

3 BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe.

5 Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja, Na neno lake nimelitumainia.

6 Nafsi yangu inamngoja Bwana, Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi, Naam, walinzi waingojao asubuhi.

7 Ee Israeli, umtarajie BWANA; Maana kwa BWANA kuna fadhili, Na kwake kuna ukombozi mwingi.

8 Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya