Zaburi 70 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba musaada ( Zab 40.13-17 ) 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea sadaka yake ya ukumbusho. 2 Ee Mungu, uniokoe! Ee Yawe, ukuje haraka unisaidie. 3 Wapate haya na kufezeheka wanaotaka kuniua! Warudi nyuma na kufezeheka wanaonitakia hasara! 4 Wapumbazike kwa haya, hao wanaofurahia kunizomea! 5 Lakini wote wanaokutafuta, wafurahi na kushangilia kwa sababu yako. Wote wanaopenda wokovu wako, waseme siku zote: “Mungu ni mukubwa!” 6 Nami ninayekuwa masikini na mukosefu, unifikie haraka, ee Mungu! Wewe ndiwe musaada wangu na mukombozi wangu. Ee Yawe, usikawie! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo