Zaburi 53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mutu asiyemwabudu Mungu 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi. 2 Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu!” Wote wamepotoka kabisa, wametenda mambo ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri. 3 Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni, aone kama kuna yeyote mwenye akili kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu. 4 Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja. 5 Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate; wala hawajali Mungu. 6 Hapo watashikwa na hofu, hofu ambayo hawajapata kuiona; maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui, hao watafezeheka maana Mungu amewakataa. 7 Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni! Mungu atakapotengeneza hali ya watu wake, wazao wa Yakobo watashangilia; watu wa Israeli watafurahi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo