Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Zaburi 53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mutu asiyemwabudu Mungu

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo wa huzuni. Mashairi ya Daudi.

2 Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu!” Wote wamepotoka kabisa, wametenda mambo ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri.

3 Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni, aone kama kuna yeyote mwenye akili kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.

4 Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.

5 Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate; wala hawajali Mungu.

6 Hapo watashikwa na hofu, hofu ambayo hawajapata kuiona; maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui, hao watafezeheka maana Mungu amewakataa.

7 Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni! Mungu atakapotengeneza hali ya watu wake, wazao wa Yakobo watashangilia; watu wa Israeli watafurahi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ