Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Zaburi 41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi ya mugonjwa

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2 Heri mutu anayeshugulikia masikini; Yawe atamwokoa wakati wa shida.

3 Yawe atamulinda na kuchunga uzima wake, naye atafanikiwa katika inchi; hatamwacha katika makucha ya waadui zake.

4 Yawe atamusaidia anapokuwa mugonjwa, atamuponyesha magonjwa yake yote.

5 Nami nilisema: “Unirehemu, ee Yawe, uniponyeshe, maana nimekukosea.”

6 Waadui zangu wanasema hivi vibaya juu yangu: “Atakufa wakati gani kusudi jina lake lisahauliwe!”

7 Wananitembelea bila kuwa na nia njema, wanawaza mabaya juu yangu, wanapofika inje wanawatangazia wengine.

8 Wote wanaonichukia wananongoneza juu yangu; wananiwazia mambo mabaya.

9 Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”

10 Hata rafiki yangu wa moyo niliyemwamini, rafiki aliyechangia chakula nami, amegeuka kunishambulia!

11 Ee Yawe, unionee huruma! Uniponyeshe, nami nitawalipiza kisasi.

12 Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami, waadui zangu wasipopata ushindi juu yangu.

13 Wewe unaniimarisha katika ukamilifu; utanichunga mbele yako milele.

14 Yawe, Mungu wa Israeli, asifiwe, tangu milele na hata milele! Amina! Amina!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ