Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Zaburi 146 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sifa kwa Mungu Mwokozi

1 Haleluia! Ee nafsi yangu, umusifu Yawe!

2 Nitamusifu Yawe maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu muda wote nitakapoishi.

3 Musiwategemee wakubwa wa dunia; hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa.

4 Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka.

5 Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,

6 aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao. Yeye anashika ahadi yake milele.

7 Yeye anawapatia wanaoonewa haki yao, anawapa wenye njaa chakula. Yawe anawapa wafungwa uhuru,

8 anawafungua vipofu macho. Yawe anawainua waliogandamizwa; anawapenda watu wa haki.

9 Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu.

10 Yawe anatawala milele. Mungu wako, ee Sayuni, ni mufalme kwa vizazi vyote! Haleluia!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ