Zaburi 146 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sifa kwa Mungu Mwokozi 1 Haleluia! Ee nafsi yangu, umusifu Yawe! 2 Nitamusifu Yawe maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu muda wote nitakapoishi. 3 Musiwategemee wakubwa wa dunia; hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa. 4 Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka. 5 Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake, 6 aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao. Yeye anashika ahadi yake milele. 7 Yeye anawapatia wanaoonewa haki yao, anawapa wenye njaa chakula. Yawe anawapa wafungwa uhuru, 8 anawafungua vipofu macho. Yawe anawainua waliogandamizwa; anawapenda watu wa haki. 9 Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu. 10 Yawe anatawala milele. Mungu wako, ee Sayuni, ni mufalme kwa vizazi vyote! Haleluia! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo