Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Masemi ya Elihu ( 32.1–37.24 ) Maneno ya mwisho ya Yobu

1 Basi hawa watu watatu: Elifasi, Bildadi na Zofari, wakaacha kumujibu Yobu kwa vile alijiona kuwa mwenye haki.

2 Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi wa ukoo wa Rama akakasirika. Alimukasirikia Yobu kwa sababu Yobu alijiona yeye mwenye haki na wala si Mungu.

3 Vilevile, aliwakasirikia warafiki watatu wa Yobu kwa sababu hawakukuwa na neno la kumujibu Yobu, na kwa hiyo wakaonyesha kwamba Mungu amekosa.

4 Elihu alikuwa amekaa kimya wakati wale wazee waliposema na Yobu kwa maana yeye alikuwa kijana kuliko wao.

5 Lakini alipoona wale watu watatu wameshindwa kumujibu Yobu, akawaka hasira.

6 Basi, Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi, akaanza kusema: Mimi ni kijana, ninyi ni wazee zaidi. Kwa hiyo niliogopa kuwaambia mawazo yangu.

7 Nilisema ndani ya moyo: “Uwaache wenye siku nyingi waseme, wenye miaka mingi wafundishe hekima.”

8 Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.

9 Si lazima kuwa muzee kusudi ukuwe na hekima; haiko wazee tu ndio wenye kufahamu jambo linalokuwa sawa.

10 Kwa hiyo ninasema: “Munisikilize, muache nami nitoe maoni yangu.”

11 Basi, mimi nilingojea kile mulichotaka kusema, nilisikiliza misemo yenu ya hekima, mulipokuwa munajaribu kutafuta neno la kusema.

12 Niliwasikiliza kwa uangalifu sana, lakini hakuna hata mumoja wenu aliyemushinda Yobu; wote mulishindwa kujibu kwa maneno yake.

13 Kwa hiyo musiseme: “Sasa tumepata hekima. Atakayemushinda ni Mungu, wala si mwanadamu.”

14 Maneno ya Yobu hayakukuwa kwa ajili yangu. Kwa hiyo sitamujibu kama vile mulivyomujibu ninyi.

15 Ninyi mumeshangaa na kukaa kimya; ninyi hamuna cha kusema zaidi.

16 Basi, ningoje tu kwa vile hamusemi, kwa sababu munakaa tu bila kujibu kitu?

17 Mimi vilevile nitatoa jibu langu; mimi nitatoa vilevile maoni yangu.

18 Niko na maneno mengi sana, roho yangu inanisukuma kusema.

19 Moyo wangu umefurika kama divai iliyozibwa, kama kibuyu cha divai mupya tayari kupasuka.

20 Ni lazima niseme kusudi nipate kutulia; inanipasa kufungua kinywa changu na kujibu.

21 Sitamupendelea mutu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mutu,

22 maana mimi sijui kubembeleza mutu. Kama si vile, Muumba wangu angeniangamiza.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ