Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.

2 Au, ninangojea nini kutoka kwa Mungu anayekuwa juu? Mungu Mwenye Uwezo ameniwekea kitu gani?

3 Hasara haipati watu waovu na maangamizi wale wanaotenda mabaya?

4 Mungu haoni njia zangu na kujua hatua zangu zote?

5-6 Mungu anipime katika mizani ya haki, naye ataona kwamba sina kosa. Kama nimeishi kwa kufuata uongo, kama nimekimbilia kudanganya watu,

7 kama hatua zangu zimepotoka nao moyo wangu ukafuata tamaa za macho yangu, kama mikono yangu imechafuliwa na zambi,

8 basi nipande na mwingine akule, mazao yangu ya shamba yaongolewe.

9 Kama moyo wangu umevutwa kwa muke wa mutu, kama nimevizia kwenye mulango wa jirani yangu,

10 basi, muke wangu amupikie mume mwingine, na wanaume wengine walale naye.

11 Jambo hilo ni kosa la kuchukiza, uovu ambao mwamuzi anapaswa kuazibu.

12 Kosa langu lingekuwa kama vile moto wa kuniteketeza na kuangamiza, na kuchoma kabisa mapato yangu yote.

13 Kama nimekataa maneno ya mutumishi au mujakazi wangu, waliponiletea malalamiko yao,

14 nitafanya nini basi Mungu atakaposimama mbele yangu? Akinichunguza, nitamujibu nini?

15 Maana Mungu ndiye aliyeniumba mimi na mutumishi wangu; yeye ndiye aliyetuumba sisi wote.

16 Nimepata kumukatalia masikini mahitaji yake au kuwafanya wajane watumaini bure?

17 Nimekula chakula changu peke yangu, bila kuwaachia wayatima nao wapate kitu chochote?

18 Hapana! Tangu ujana wangu nimekuwa baba yao aliyewalea, tangu utoto wangu nimewaongoza wajane.

19 Nilipoona mutu anakufa kwa kukosa nguo, au masikini ambaye hana nguo ya kuvaa,

20 nilimupa joto kwa nguo za manyoya ya kondoo wangu naye akanitakia baraka za shukrani ya moyo.

21 Kama nimekunjia yatima ngumi katika tribinali nikijua nitapendelewa na waamuzi,

22 basi, bega langu liongoke, mukono wangu ukwanyuke kwenye maungio yake.

23 Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.

24 Sikuweka tumaini langu katika zahabu, sikuiambia zahabu safi: “Wewe ni usalama wangu”,

25 sikupata kufurahia wingi wa utajiri wangu au kujivunia mapato mengi ya mikono yangu.

26 Sikuangalia jua likiangaza au mwezi ukipita katika uzuri wake

27 kusudi niviabudu kwa siri, na kubusu mikono yangu kwa heshima yake.

28 Huo ungekuwa uovu wa kuazibiwa na waamuzi maana ningekuwa mwongo mbele ya Mungu anayekuwa juu.

29 Nimefurahia kuangamia kwa adui yangu, au kufurahi alipopatwa na hasara?

30 Hapana! Sikuruhusu kinywa changu kusema mabaya juu yake, kwa kumulaani kusudi akufe.

31 Watumishi wangu wote wanasema wazi, kila mugeni amekaribishwa katika nyumba yangu.

32 Musafiri hakulala inje ya nyumba yangu; nilimufungulia mulango mupita njia.

33 Nimeficha makosa yangu kama wengine? Nimekataa kutambua zambi zangu?

34 Sijaogopa kusimama mbele ya kundi la watu wala kukaa kimya au kujifungia ndani, kwa kuogopa kutishwa na mazarau yao.

35 Heri kungekuwa mutu wa kunisikiliza! Ninaweza kutia sahihi yangu katika kila neno nililosema. Mungu Mwenye Uwezo anijibu! Heri mashitaki waadui zangu wanayonitolea yangeandikwa!

36 Ningeyabeba kwa sifa juu ya mabega yangu na kuyavaa kwenye kichwa kama taji.

37 Ningemuhesabilia Mungu kila kitu nilichofanya, ningemwendea kama mwana wa mufalme.

38 Kama nimeiba shamba ninalolima na kusababisha mifereji yake iomboleze,

39 kwa kufaidika na mazao yake bila kulipa na kusababisha kifo cha wenyeji,

40 basi miiba iote mule pahali pa ngano, na magugu pahali pa shayiri. Mwisho wa masemi ya Yobu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ