Yobu 30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo. 2 Ningepata faida gani katika mikono yao, watu ambao nguvu zao zilikuwa zimewaishia? 3 Katika ukosefu na njaa kali walitafutatafuta kitu cha kutafuna katika jangwa, sehemu tupu zisizokuwa na chakula. 4 Walichuma mimea katika jangwa na majani katika pori wakakula, walikula hata mizizi ya muti wa vifagio. 5 Walifukuzwa mbali na watu, watu waliwapigia kelele kama wezi. 6 Iliwapasa kutafuta usalama katika mifereji kwenye maporomoko, katika mashimo ndani ya udongo na mawe. 7 Kule katika vichaka walilia kama nyama, walikusanyika pamoja chini ya nyasi. 8 Walikuwa wapumbafu wakubwa na waovu ambao walilazimishwa kufukuzwa katika inchi kwa fimbo. 9 Na sasa wamenitungia wimbo wa kunizomea, nimekuwa kitu cha kuchekesha kwao. 10 Wananichukia na kuniepuka; wakiniona tu wanatema mate kwenye uso. 11 Kwa maana Mungu ameniregeza na kunishusha, wamekuwa huru kunitendea wanavyopenda. 12 Kundi la watu linasimama kwa kunishitaki, likitafuta kuniangusha kwa kunitegea. Linanishambulia kusudi niangamie. 13 Watu hao wanakata njia yangu, wanazidisha hasara yangu, na hakuna mutu wa kuwazuia. 14 Wanakuja kama kwenye njia kubwa, na kisha mashambulio wanasonga mbele. 15 Hofu kubwa imenishika. Heshima yangu imetoweka kama kwa upepo, na raha yangu imepita kama wingu. 16 Sasa sina nguvu yoyote ndani ya nafsi yangu; siku za mateso zimenipata. 17 Usiku mifupa yangu yote inauma; maumivu yanayonitafuna hayapoi. 18 Mungu amenishika kwa nguo zangu, amenibana kama shingo ya kanzu yangu. 19 Amenitupa katika matope; nimekuwa kama majivu na mavumbi. 20 Ninakulilia, lakini haunijibu, ninasimama kuomba lakini haunisikilizi. 21 Umegeuka kuwa mukali kwangu, unanitesa kwa mukono wako wenye nguvu. 22 Unanitupa katika upepo na kunipeperusha; unanitupatupa huku na kule katika zoruba kali. 23 Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana. 24 Basi, mutu akiangamia hainui mukono? Mutu akiwa tabani haombi musaada? 25 Sikuwalilia wale waliokuwa na taabu? Sikuona uchungu kwa ajili ya wamasikini? 26 Lakini nilipotazamia mazuri, mabaya yalinipata; nilipongojea mwangaza, giza lilikuja. 27 Moyo wangu unahangaika wala hautulii hata kidogo. Siku za mateso zimenipata. 28 Ninapitapita nikiomboleza. Kwangu hakuna jua. Ninasimama katika makutano kuomba musaada. 29 Kwa kilio nimekuwa ndugu ya imbwa wa pori, kati ya mimi na mbuni hakuna tofauti. 30 Ngozi yangu inakuwa nyeusi na inachubuka, mifupa yangu inaungua kwa homa. 31 Kinubi changu kimekuwa cha kufanya kilio filimbi yangu kwa ajili ya kuomboleza. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo