Yobu 27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Yobu akaendelea kutoa masemi yake, akasema: 2 Kama vile Mungu anavyoishi, aliyeniondolea haki yangu, Mungu Mwenye Uwezo aliyeifanya nafsi yangu ikuwe na uchungu, 3 ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu, 4 midomo yangu haitasema uongo hata kidogo, wala ulimi wangu kusema udanganyifu. 5 Siwezi kabisa kusema kwamba ninyi munasema ukweli. Mpaka kufa kwangu ninasema sina kosa. 6 Ninashikilia haki yangu, wala sitaiacha; katika zamiri yangu sina cha kunihukumu katika maisha yangu. 7 Adui yangu apate azabu ya mwovu, anayesimama kunishambulia aazibiwe kama mubaya. 8 Asiyemwogopa Mungu ana tumaini gani wakati Mungu anapokata pumzi yake, anapomwondolea uzima wake? 9 Wakati atakapopatwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake? 10 Mwovu hawezi kufurahi mbele ya Mungu Mwenye Uwezo; hataweza kudumu akimwomba Mungu. 11 Nitawafundisha jinsi kitendo cha Mungu kinavyokuwa, sitawaficha mipango ya Mungu Mwenye Uwezo. 12 Lakini ninyi munajua jambo lile vizuri sana! Mbona, basi munasema maneno yasiyokuwa na maana? 13 Hiki ndicho Mungu alichomwekea mutu mwovu; mutesaji alichopangiwa kupata ni hiki: 14 Watoto wake hata wakuwe wengi watauawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa na chakula cha kutosha. 15 Wale watakaopona watakufa kwa ugonjwa mukali, na wajane wao hawatawaomboleza. 16 Hata akilundika feza kama vile mavumbi, na nguo kama vile udongo wa mufinyanzi, 17 yeye alundike tu, lakini mwenye haki ndiye atakayezivaa, na feza yake watu wasiokuwa na kosa wataigawanyana. 18 Nyumba mwovu anayojenga ni kama vile utando wa buibui, ni kama vile kibanda cha mulinzi katika shamba. 19 Anakwenda kulala akiwa tajiri, lakini ni mara ya mwisho; atafungua macho yake, na utajiri wake umetoweka! 20 Vitisho vinamufikia kama vile mafuriko; usiku anapatwa na zoruba. 21 Upepo mukali wa mashariki unamupeperusha naye anatoweka; unamufagilia mbali kutoka makao yake. 22 Upepo ule unamufunika bila huruma; anajaribu kukimbia lakini mbio za bure. 23 Upepo unamupigia vigelegele anapokimbia, na kumuzomea toka pahali pake. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo