Yobu 26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Jibu la Yobu 1 Kisha Yobu akajibu: 2 Aa! Jinsi gani ulivyomusaidia asiyekuwa na uwezo! Jinsi gani ulivyomwokoa asiyekuwa na nguvu! 3 Jinsi gani ulivyomushauri asiyekuwa na hekima, na kumushirikisha ujuzi wako! 4 Lakini umesema hayo kwa ajili ya nani? Nani aliyekusukuma kuongea hivyo? Bildadi anasema 5 Mizimu kule chini inatetemeka, maji ya chini na wakaaji wake yanaogopa. 6 Kuzimu kuko wazi kabisa mbele ya Mungu. Shimo la kuangamia halina kifuniko chochote. 7 Mungu anatandaza kaskazini juu ya pahali patupu, na anatundika dunia pahali pasipo kuwa kitu. 8 Anayafunga maji katika mawingu yakuwe mazito, nayo mawingu hayapasuki kwa uzito wake. 9 Anaufunika uso wa mwezi na kutandaza juu yake wingu. 10 Amechora muviringo juu ya uso wa bahari, penye mpaka kati ya mwangaza na giza. 11 Mungu akitoa sauti ya kukaripa, nguzo za mbingu zinatetemeka na kushangaa. 12 Kwa nguvu zake alituliza bahari; kwa maarifa yake alimwangamiza Rahabu. 13 Kwa pumzi yake alisafisha anga; mukono wake ulitoboa nyoka mukubwa anayeruka. 14 Ikiwa haya ni machache tu ya matendo yake, ni minongono tu tunayosikia juu yake, nani anayeweza kujua ukubwa wa nguvu yake? |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo