Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sehemu ya tatu ya Mazungumuzo ( 22.1–27.23 ) Masemi ya Elifasi

1 Kisha Elifasi wa inchi ya Temani akajibu Yobu:

2 Mwanadamu anafaa kwa kitu chochote mbele ya Mungu? Kwa kweli mwenye hekima anajifaidia mwenyewe tu.

3 Unazani kwamba unamufurahisha Mungu Mwenye Uwezo kama wewe ni mwenye haki? Au anapata faida gani kama uko mukamilifu?

4 Unazani anakuazibu na kukuhukumu kwa sababu wewe unamuheshimu?

5 Hapana! Uovu wako ni mukubwa sana! Ubaya wako hauna mwisho!

6 Wewe umemunyanganya ndugu yako nguo ya rehani; umemutwaa nguo hiyo moja anayokuwa nayo.

7 Umewanyima maji wale waliokuwa wamechoka; umewanyima chakula wale wanaokuwa na njaa.

8 Umemuruhusu mwenye cheo kunyanganya inchi yote; umemwacha anayependelewa aishi mule.

9 Umewaacha wajane waende mikono mitupu; umewaponda wayatima mikono yao.

10 Kwa hiyo mitego imekuzunguka pande zote, hofu ya rafla imekupata.

11 Giza limekuangukia usione kitu; mafuriko ya maji yamekufunika.

12 Tunajua kwamba Mungu yuko kule juu mbinguni; Angalia jinsi nyota za juu kabisa zinavyokuwa mbali!

13 Lakini wewe unasema: “Mungu anajua nini? Anaweza kupenya mawingu na kutoa hukumu?

14 Mawingu mazito yamemuzunguka asipate kuona; anatembea inje ya anga la dunia!”

15 Umeamua kufuata njia za zamani ambazo watu waovu wamezifuata?

16 Hao walifagiliwa mbele ya wakati wao, misingi yao imepelekwa mbali na maji.

17 Hao ndio waliomwambia Mungu: “Achana nasi!” Na “Wewe Mungu Mwenye Uwezo unaweza nini juu yetu?”

18 Lakini Mungu ndiye aliyejaza nyumba zao fanaka, lakini walimuweka mbali na mipango yao!

19 Wenye haki wanaona na kufurahi, wasiokuwa na kosa wanawachekelea.

20 Wanasema: kweli wale waadui zetu wameangamizwa, na walichoacha kimeteketezwa kwa moto.

21 Sasa, Yobu, ukubaliane na Mungu ukuwe na amani, na kwa hiyo mazuri yatakufikia.

22 Pokea mafundisho kutoka kwake; na uyaweke maneno yake ndani ya moyo wako.

23 Ukimurudilia Mungu na kunyenyekea, ukiondoa uovu mbali na makao yako,

24 ukitupilia mbali mali yako, ukitupa zahabu ya Ofiri kwenye ukingo wa kijito,

25 Mungu Mwenye Uwezo akiwa ndiyo zahabu yako na feza yako ya bei kali,

26 basi, ndipo utakapomufurahia Mungu Mwenye Uwezo na kuinua uso wako kwake.

27 Utamwomba naye atakusikiliza, nawe utavitimiza viapo vyako.

28 Neno lolote utakalokusudia litafanikiwa, na mwangaza utaangazia njia zako.

29 Maana, Mungu anawashusha wenye majivuno, lakini anawaokoa wanyenyekevu.

30 Yeye anamwokoa mutu asiyekuwa na kosa. Nawe utaokolewa kwa sababu haukutenda mabaya.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ