Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Yobu akajibu:

2 Musikilize kwa uangalifu maneno yangu; na hiyo ikuwe ndiyo faraja yenu.

3 Munivumilie, nami nitasema, na nikisha sema muendelee kunichekelea.

4 Basi, mimi ninamulalamikia mwanadamu? Kwa nini basi nikose uvumilivu?

5 Muniangalie, nanyi mushangae, muweke mikono yenu juu ya vinywa vyenu.

6 Nikifikiri yaliyonipata ninafazaika, mwili wangu unatetemeka kwa hofu.

7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi? Mbona nguvu zao zinaongezeka hata katika uzee?

8 Wanaona watoto wao wakifanikiwa na wazao wao wakipata nguvu.

9 Kwao kila kitu ni salama bila hofu, wala fimbo ya Mungu haiwafikii.

10 Kweli, ngombe wao wote wanaongezeka, wanazaa bila matatizo yoyote.

11 Watoto wao wachanga wanatembea kama kundi; na watoto wao wanacheza ngoma;

12 wanacheza muziki wa ngoma na vinubi, na kufurahia sauti ya filimbi.

13 Wanaishi maisha ya fanaka kisha wanashuka kwa amani katika kuzimu.

14 Wanamwambia Mungu: “Usitusumbue! Hatutaki kujua mapenzi yako.

15 Mungu Mwenye Uwezo ni nini hata tumutumikie? Tunapata faida gani tukimwomba?”

16 Kufanikiwa kwao si kuko katika mikono yao, wakiwa wamemuweka Mungu mbali na mipango yao?

17 Mara ngapi umepata kuona mwangaza wa maisha ya mwovu umezimishwa na kupatwa na hasara? Au Mungu amekwisha kuwaangamiza kwa hasira yake?

18 Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka, wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!

19 Ninyi munasema: “Mungu amewawekea watoto wao azabu ya watu wale waovu.” Kwa nini hawalipizi wao wenyewe, wapate kutambua?

20 Waone wenyewe maangamizi yao; waone wenyewe kasirani ya Mungu Mwenye Uwezo.

21 Maana siku zao zitakapokwisha, watajali nini juu ya wazao wao?

22 Mwanadamu anaweza kumufundisha Mungu maarifa, Mungu ambaye anahukumu wakaaji wa mbinguni?

23 Mutu mumoja anakufa mwenye nguvu tele, akiwa katika raha na salama,

24 akijaa mafuta tele katika mwili, na mifupa yake ikiwa bado na nguvu.

25 Mwingine anakufa na huzuni kubwa ndani ya moyo, akiwa hajaonja bado jambo lolote jema.

26 Hata hivyo, wote wanakufa na kuzikwa, wote wanafunikwa na vidudu.

27 Musikilize! Mimi ninajua mawazo yenu yote, na mipango yenu ya kunizarau.

28 Ninyi munauliza: “Iko wapi nyumba ya yule mukubwa? Iko wapi nyumba mwovu alimoishi?”

29 Hamujawauliza wapita njia? Hamukufahamu habari zao?

30 Mwovu anaponyeshwa siku ya hasara, anaokolewa siku ya kasirani!

31 Ni nani atakayemwonyesha makosa yake, au atakayemulipa kwa yote aliyotenda?

32 Anapokamatwa kupelekwa katika kaburi, kaburi lake linalindwa.

33 Nyuma yake watu wengi wanamusindikiza na wengine wengi sana wanamutangulia. Anapozikwa, udongo unateremushwa polepole.

34 Mutaweza namna gani basi, kunifariji kwa maneno matupu? Majibu yenu hayana kitu chochote lakini uongo tu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ