Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Bildadi, wa inchi ya Suhi, akajibu:

2 Utawinda maneno ya kusema mpaka wakati gani? Fikiri vizuri nasi tutasema.

3 Kwa nini unatufanya kama ngombe? Mbona unatuona sisi kuwa wapumbafu?

4 Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako. Dunia itaachwa tupu kwa ajili yako au mawe yahamishwe toka pahali pake?

5 Kweli, mwangaza wa mutu mwovu utazimishwa; ulimi wa moto wake hautaangaa.

6 Katika nyumba yake mwangaza ni giza, taa inayomwangazia itazimishwa.

7 Hatua zake ndefu zitafupishwa; mipango yake itamwangusha chini.

8 Miguu yake mwenyewe itamutia katika mutego; kila mara anatembea juu ya shimo.

9 Mutego unamukamata kwenye kisigino, kamba inamunasa kabisa.

10 Amefichiwa kamba ya kumunasa ndani ya udongo, ametegewa mutego katika njia yake.

11 Hofu kubwa inamutisha kila upande, inamufuata katika kila hatua yake.

12 Alikuwa na nguvu, lakini sasa njaa imemubana; hasara ziko tayari kumwangusha.

13 Ugonjwa mukali unakula ngozi yake, ugonjwa wa kifo unaharibu viungo vyake.

14 Anaongolewa katika nyumba aliyotegemea, na kupelekwa kwa mufalme wa vitisho.

15 Nyumba yake tupu, wengine wataishi ndani; kiberiti kimetawanywa katika makao yake.

16 Yeye ni kama muti uliokauka mizizi, matawi yake juu yamenyauka.

17 Katika inchi hakuna atakayemukumbuka; jina lake halitatamkwa tena katika barabara.

18 Ameondolewa toka katika mwangaza, akatupwa katika giza; amefukuzwa mbali kutoka katika dunia.

19 Hana watoto wala wajukuu; hakuna aliyebaki katika makao yake.

20 Watu wa upande wa magaribi wameshangazwa na yaliyomupata; hofu imewapata watu wa upande wa mashariki.

21 Hayo ndiyo yanayowapata wasiomujali Mungu; pale ndipo pahali pa wasiomujua Mungu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ