Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nimevunjika moyo, siku zangu zimekwisha, kaburi langu liko tayari.

2 Kweli wanaonichekelea wamenizunguka, matusi yao yananizuiza kulala.

3 Ee Mungu, ujitoe mwenyewe kuwa rehani kwa ajili yangu maana hakuna mwingine wa kujitoa kwa ajili yangu.

4 Umefumba akili za warafiki zangu; usiwaache basi wanishinde.

5 Mutu anayefitini warafiki zake kwa faida, watoto wake watakufa macho.

6 Nimefanywa kuwa kichekesho kwa watu, nimekuwa mutu wa kutemewa mate.

7 Macho yangu yamefifia kwa ajili ya uchungu; viungo vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.

8 Watu wa haki wanashangaa wanapoona hayo, nao wasiokuwa na kosa wanachukizwa na wasiomwogopa Mungu.

9 Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.

10 Lakini ninyi mukuje, mukuje wote tena. Kwenu sitamupata mwenye hekima hata mumoja.

11 Siku zangu zimekwisha, mipango yangu imevunjwa, matazamio ya moyo wangu yametoweka.

12 Kwa hao watu, usiku ni muchana: wanasema kwamba mwangaza unakaribia giza.

13 Kama kuzimu kukiwa nyumba yangu, na makao yangu yako kule katika giza,

14 kama nikiita kaburi “baba yangu” na vidudu “mama yangu” au “dada yangu”,

15 basi, nimebakiliwa na tumaini gani? Ni nani anayeweza kuona tumaini lile?

16 Tazamio langu litashuka nami kuzimu! Tutateremuka wote wawili mpaka kule katika mavumbi!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ