Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Yobu 13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sikia! Hayo yote nimeyaona kwa macho yangu. Nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.

2 Yote munayoyajua, mimi vilevile ninayajua. Mimi si mutu wa akili ndogo kuliko ninyi.

3 Lakini ningependa kusema na Mungu Mwenye Uwezo, ninatamani kujitetea mbele ya Mungu.

4 Lakini ninyi munapakaa uongo chokaa, ninyi wote ni waganga wasiofaa kitu.

5 Heri mungekaa kimya kabisa, muonekane kwamba muna hekima!

6 Musikilize basi utetezi wangu, munisikilize ninapojitetea.

7 Munazani munamutumikia Mungu kwa kusema uongo na udanganyifu?

8 Munajaribu kumupendeza Mungu? Mutamutetea Mungu katika tribinali?

9 Akiwachunguza, ninyi mutapona? Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?

10 Hakika yeye atawakaripia kama mukionyesha upendeleo kwa siri.

11 Utukufu wake hauwatishi? Hamupatwi na hofu juu yake?

12 Masemi yenu ni mezali za majivu, maneno yenu ni ukuta wa udongo.

13 Munyamaze, nami niseme. Kitu kitakachonipata, kinipate.

14 Niko tayari hata kuhatarisha maisha yangu.

15 Mungu aniue akitaka; sina la kupoteza. Hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.

16 Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.

17 Musikilize kwa uangalifu maneno yangu, maelezo yangu yatue katika masikio yenu.

18 Maneno yangu nimeyatarisha jinsi inavyofaa. Ninajua kwamba sina kosa.

19 Nani atakayebishana nami? Niko tayari kunyamaza na kufa.

20 Mungu wangu, unijalie tu mambo haya mawili, nami sitajificha mbali na wewe:

21 kwanza uniondolee mukono wako unaonipiga, na usiniogopeshe kwa kitisho chako.

22 Uanze kusema maneno yako nami nikujibu. Au mimi nianze, nawe unijibu.

23 Makosa na zambi zangu ni ngapi? Unijulishe kosa na zambi yangu.

24 Mbona unageuza uso wako mbali nami? Kwa nini unanitendea kama adui yako?

25 Utatikisatikisa jani linalopeperushwa, au kukimbiza nyasi iliyokauka?

26 Wewe umetoa mashitaki makali juu yangu, na kunibebesha zambi za ujana wangu.

27 Unanifunga minyororo kwenye miguu, unachunguza njia zangu zote, umeichapa miguu yangu.

28 Nami ninaisha kama muti uliooza, kama nguo iliyokuliwa na nondo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ