Yeremia 47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Neno la Yawe juu ya Wafilistini Misri inashambuliwa 1 Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza: 2 Yawe anasema hivi: Maji yanapanda kutoka kaskazini, nayo yatakuwa muto uliofurika; yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake, muji na wakaaji na wanaoishi humo. Watu watalia, wakaaji wote wa inchi wataomboleza. 3 Watasikia shindo la kwato za farasi, kelele za magari ya vita, na vishindo vya magurudumu yao. Wababa watawasahau watoto wao, mikono yao itakuwa imeregea sana. 4 Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote, kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona. Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini, watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori. 5 Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza; muji wa Askeloni umeangamia. Enyi watu muliobaki katika bonde mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani? 6 Ee upanga wa Yawe! Utatwaa muda gani ndipo utulie? Ingia katika mufuko wako, upate kutulia na kunyamaza! 7 Lakini utaweza kutulia namna gani, ikiwa ni Yawe ameupa kazi? Ameuamuru ushambulie muji wa Askeloni na watu wanaoishi kandokando ya bahari. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo