Waroma 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuishi chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu 1 Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo. 2 Maana sheria ya Roho anayepana uzima kwa kuungana na Yesu Kristo imetuweka kuwa huru kutoka sheria ya zambi na ya kifo. 3 Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi. 4 Alifanya vile kusudi maagizo ya haki ya Sheria yapate kutimizwa ndani yetu sisi tunaoishi kufuatana na uongozi wa Roho wa Mungu, lakini si kufuatana na hali yetu ya kimwili. 5 Kwa maana wale wanaoishi kwa kufuatana na hali ya kimwili, wanashugulika na mambo yanayotakiwa na mwili lakini wale wanaoishi kufuatana na uongozi wa Roho wa Mungu wanashugulika na mambo yanayotakiwa na Roho yule. 6 Kushugulika na mambo yanayotakiwa na hali ya kimwili kunaleta kifo lakini kushugulika na mambo yanayotakiwa na Roho wa Mungu kunaleta uzima na amani. 7 Kwa maana wale wanaoshugulika na hali ya kimwili ni waadui za Mungu; hawatii sheria ya Mungu wala hawawezi kuitii. 8 Watu wanaotawaliwa na hali ya kimwili hawawezi kumupendeza Mungu. 9 Lakini ninyi sasa hamutawaliwi na hali yenu zaifu ya kimwili, lakini munatawaliwa na Roho Mutakatifu, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Na mutu yeyote asiyekuwa na Roho wa Kristo ndani yake, yeye si mutu wa Kristo. 10 Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, ijapokuwa mwili wenu unakufa kwa sababu ya zambi, Roho ndiye uzima wenu kwa maana munahesabiwa haki mbele ya Mungu. 11 Na kama Roho wa Mungu aliyemufufua Yesu anakaa ndani yenu, basi huyo aliyemufufua Kristo ataupatia mwili wenu unaokuwa wa kufa uzima kwa njia ya Roho wake anayekaa ndani yenu. 12 Basi wandugu, tuko na deni, lakini si la kutimiza mapaswa ya hali yetu ya kimwili hata tuishi kufuatana na hali ile. 13 Kwa maana kama mukiishi kufuatana na hali ya kimwili, mutakufa. Lakini kama mukiua matendo mabaya ya mwili kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, mutaishi. 14 Wote wanaoishi chini ya uongozi wa Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu. 15 Kwa maana hamukupewa roho anayewafanya muishi katika utumwa na kuwatia tena woga, lakini mulipewa Roho anayewafanya mukubaliwe kuwa watoto wa Mungu. Na kwa uwezo wa Roho huyo, tunaweza kumwita Mungu “Baba.” 16 Roho huyo mwenyewe anahakikisha ndani ya roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. 17 Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile. Utukufu utakaokuja 18 Ninaona kwamba mateso ya wakati huu wa sasa hayawezi kupima kulinganishwa na utukufu ambao Mungu atakaoonyesha kwetu waziwazi. 19 Viumbe vyote vinangojea kwa hamu sana wakati Mungu atakapowaonyesha watoto wake waziwazi. 20 Kwa maana viumbe vyote vimewekwa chini ya utawala wa mambo ya ovyo, si kwa mapenzi yao, lakini kwa sababu ya yule aliyewatia katika hali hiyo. Lakini kungali tumaini hili: 21 siku moja viumbe hivi vitawekwa huru toka katika utumwa wa uharibifu na kushiriki katika uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu. 22 Kwa maana tunajua kwamba mpaka sasa viumbe vyote vinaugua kwa uchungu kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa. 23 Na si viumbe hivi tu; hata sisi tuliokwisha kuwa na Roho wa Mungu kama sehemu ya kwanza ya zawadi Mungu atakazotoa, tunaugua vilevile ndani yetu, tukingojea kukubaliwa na Mungu kuwa watoto wake, maana yake kukombolewa kwa kimwili. 24 Kwa maana tumeokolewa, lakini ni kwa tumaini. Mutu akiona kitu anachokitumainia, hilo si tumaini tena, kwa maana nani anayeweza kuendelea kutumainia kitu anachokiona? 25 Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu. 26 Na ni hivi vilevile Roho wa Mungu anatusaidia katika uzaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba sawa inavyopaswa. Lakini Roho wa Mungu yeye mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa kuugua kusikoweza kuelezwa. 27 Na Mungu anayeona yanayokuwa ndani ya mioyo yetu, anajua nia ya Roho Mutakatifu, kwa maana Roho anawaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu. 28 Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake. 29 Kwa maana wale Mungu aliowachagua tangu zamani, ndio aliofanya mupango juu yao tangu zamani, apate kuwafananisha na Mwana wake, kusudi Mwana wake akuwe muzaliwa wa kwanza wa wandugu wengi. 30 Na wale Mungu aliowachagua tangia zamani, aliwaita vilevile; nao aliowaita, akawahesabia haki, nao aliowahesabia haki, akawatukuzisha vilevile. Ukubwa wa upendo wa Mungu 31 Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi? 32 Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake? 33 Ni nani anayeweza kuwashitaki watu ambao Mungu alijichagulia? Hakuna hata mumoja! Mungu peke yake amewahesabia haki mbele yake. 34 Ni nani anayeweza basi kuwahukumu? Hakuna hata mumoja! Maana Yesu Kristo ndiye aliyekufa, na zaidi ya hiyo, alifufuka, na sasa anakaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, na yeye ndiye anayetuombea. 35 Ni nani anayeweza kututenga na upendo wa Kristo? Ni taabu, au huzuni, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo? 36 Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kwa sababu yako tunauawa kila siku. Tunahesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.” 37 Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda. 38 Kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kinachoweza kututenga na upendo wa Mungu: wala kifo, wala uzima, wala wamalaika, wala watawala, wala mambo ya sasa, wala mambo yatakayokuja, wala wenye uwezo, 39 wala nguvu za juu, wala nguvu za chini, wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu aliouonyesha kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo