Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Waroma 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kristo ametupatanisha na Mungu

1 Sasa kufuatana na vile tumekwisha kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani, kunakuwa sasa amani kati yetu na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

2 Kwa njia ya imani, Yesu ametuwezesha kukaribia neema ya Mungu, inayokuwa musingi wetu. Sababu hii tunafurahi tukiwa na tumaini la kushiriki katika utukufu wa Mungu.

3 Zaidi ya hii, tunafurahi vilevile kwa ajili ya mateso tunayopata, kwa sababu tunajua kwamba mateso yanaleta uvumilivu,

4 na uvumilivu unaleta uaminifu kamili na uaminifu ule unaleta tumaini.

5 Nalo tumaini hili si la udanganyifu, kwa sababu Mungu amemimia upendo wake ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.

6 Kwa maana tulipokuwa hatuna uwezo wowote, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu kwa wakati uliopangwa.

7 Ni vigumu kwa mutu kukubali kufa kwa ajili ya mwenye haki. Labda mutu anaweza kujitolea kufa kwa ajili ya mutu mwema.

8 Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.

9 Sasa kwa kuwa tumehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya damu ya Yesu, inaonyesha zaidi sana kwamba atatuokoa kusudi kasirani ya Mungu isituangukie.

10 Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.

11 Wala si ile tu, lakini tunafurahi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo aliyetupatanisha sasa na Mungu.


Adamu na Kristo

12 Kwa njia ya mutu mumoja zambi iliingia katika dunia, nayo zambi ikaleta kifo. Ni hivi vilevile kifo kimefikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi.

13 Kulikuwa zambi katika dunia mbele hakujakuwa Sheria, na kwa muda Sheria ilipokuwa haijakuwa, Mungu hakuhesabu zambi.

14 Lakini kifo kilitawala tangia wakati wa Adamu mpaka wakati wa Musa, hata juu ya wale wasiofanya zambi kwa kuvunja amri, sawa vile Adamu alivyofanya. Naye ni mufano wa yule aliyengojewa kuja.

15 Lakini kuna tofauti kubwa kati ya zawadi ya Mungu na kosa la Adamu. Kwa maana ikiwa kosa la mutu mumoja lilisababisha kifo cha watu wengi, inaonyesha zaidi sana kwamba Mungu amezidisha neema yake kwa ajili ya watu wengi na zawadi inayotokana nayo kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.

16 Tena, kuna tofauti kati ya zawadi ya Mungu na mambo yaliyotokea kwa sababu ya zambi ya yule mutu mumoja. Kwa maana hukumu iliyosababishwa na zambi ya mutu mumoja, ilileta azabu, lakini zawadi ya neema ambayo Mungu alitoa kisha makosa mengi, ilileta kuhesabiwa haki mbele yake.

17 Ni kweli kwamba kifo kilitawala kwa njia ya mutu mumoja, kwa sababu ya kosa la huyo mumoja. Lakini inaonyesha zaidi sana kwamba wale wanaopewa neema ya Mungu kwa uwingi na zawadi ya haki yake, wataishi na kutawala kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.

18 Basi kama vile kosa la mutu mumoja limewaletea watu wote azabu, ni hivi vilevile tendo la haki la mutu mumoja limewaweka huru na kuwapa uzima.

19 Na kama vile kutokana na uasi wa mutu mumoja, watu wengi wamekuwa wenye zambi, ni hivi vilevile kutokana na utii wa mutu mumoja, watu wengi watahesabiwa haki mbele ya Mungu.

20 Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.

21 Hivi kama vile zambi ilivyotawala na kuleta kifo, hivi vilevile neema ya Mungu itawale kwa njia ya haki na kuleta uzima wa milele, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ