Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Walawi 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sadaka za amani

1 Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.

2 Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja kwenye mulango wa hema la mukutano. Hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.

3 Mafuta yote yanayofunika na yanayokuwa juu ya matumbotumbo ya nyama wa sadaka hiyo ya amani atayateketeza kama sadaka Yawe anayotolewa kwa moto.

4 Atatoa vilevile zile figo mbili na mafuta yake pamoja na ile sehemu bora ya maini.

5 Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.

6 Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.

7 Kama mutu atatoa mwana-kondoo kuwa sadaka yake, basi atamutolea mbele ya Yawe,

8 akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Makuhani wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.

9 Kisha, kutoka katika sadaka hiyo ya amani Yawe anayotolewa kwa moto, atamutolea sehemu hizi: mafuta yake, mukia muzima wenye mafuta uliokatwa karibu kabisa na uti wa mugongo pamoja na mafuta yote yanayofunika matumbotumbo na mafuta yote yanayokuwa kwenye matumbotumbo,

10 zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya maini.

11 Kuhani ataviteketeza hivyo vyote juu ya mazabahu kama vile chakula Yawe anachotolewa kwa moto.

12 Kama sadaka yake ni mbuzi, basi atamutolea mbele ya Yawe

13 akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.

14 Kisha, atamutolea Yawe mafuta yote yanayofunika matumbotumbo

15 na zile figo mbili na mafuta yake pamoja na sehemu bora ya maini.

16 Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.

17 Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ