Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Walawi 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Nyama wanaoruhusiwa kukuliwa na wasioruhusiwa kukuliwa
( Kumb 14.3-21 )

1 Yawe akawaambia Musa na Haruni:

2 Wawaambie Waisraeli hivi:

3 Kati ya nyama wote katika dunia, mumeruhusiwa kula nyama yeyote mwenye kwato zinazogawanyika sehemu mbili na ambaye anacheua.

4 Lakini musikule nyama yeyote ambaye anacheua lakini kwato zake hazigawanyiki sehemu mbili, au ambaye kwato zake zimegawanyika lakini hacheui. Musikule ngamia, maana anacheua lakini kwato zake hazigawanyiki sehemu mbili. Kwenu huyo ni muchafu.

5 Musikule wibari. Yeye anacheua lakini kwato zake hazigawanyiki. Kwenu huyo ni muchafu.

6 Musikule sungura. Yeye anacheua lakini kwato zake hazigawanyiki. Kwenu huyo ni muchafu.

7 Musikule nguruwe. Yeye ana kwato zinazogawanyika lakini hacheui. Kwenu huyo ni muchafu.

8 Kwa sababu nyama hao ni wachafu, musikule nyama yao wala musiguse mizoga yao.

9 Samaki yeyote wa bahari au muto mwenye mapezi na magamba, munaweza kumukula.

10 Lakini chochote kinachoishi katika bahari au ndani ya mito, ambacho hakina mapezi wala magamba, maana viumbe vyote vinavyotembea ndani ya maji na viumbe vingine vyote vinavyoishi ndani ya maji ni vichafu kwenu.

11 Viumbe hivyo vitakuwa siku zote vichafu kwenu. Musikule nyama yao, wala musiguse mizoga yao maana ni chafu.

12 Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba ni kichafu kwenu.

13 Ndege hawa wote ni wachafu kwenu. Kwa hiyo, musiwakule: tai, furukombe, kipungu,

14 mwewe, aina zote za kozi,

15 aina zote za kibombobombo,

16 mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga,

17 bundi, munandi, bundi kubwa,

18 mumbi, mwari, muderi,

19 korongo, aina zote za koikoi, hudihudi na popo.

20 Wadudu wote wenye mabawa na wanaotembea kwa miguu mine, hao ni wachafu kwenu.

21 Lakini, kati ya wadudu wenye mabawa na wanaotembea kwa miguu mine mirefu kwa kurukia juu ya udongo munaweza kula.

22 Hao ni: kila aina ya nzige, kila aina ya senene, kila aina ya panzi na kila aina ya parare.

23 Lakini wadudu wengine wote wenye mabawa na miguu mine ni wachafu kwenu.

24 Kugusa nyama fulanifulani kunamufanya mutu kuwa muchafu. Yeyote atakayegusa mizoga yao atakuwa muchafu mpaka magaribi.

25 Mutu akitwaa sehemu ya mizoga yake atakuwa muchafu mpaka magaribi na nguo zake zinapaswa kufuliwa.

26 Mutu yeyote akigusa nyama mwenye kwato zinazogawanyika lakini hacheui, mutu yule atakuwa muchafu.

27 Nyama wote wanaotembelea kwa vitanga vyao ingawa wana miguu mine, ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa muzoga wa nyama kama huyo atakuwa muchafu mpaka magaribi.

28 Mutu yeyote anayebeba muzoga atakuwa muchafu mpaka magaribi, naye atasafisha nguo zake. Hao ni wachafu kwenu.

29 Viumbe hivi ni vichafu kwenu: fuko, panya, kila aina ya mujusi,

30 guruguru, kenge, mijusi, mbulu, na kigeugeu.

31 Hao wote ni wachafu kwenu na yeyote atakayegusa mizoga yao, atakuwa muchafu mpaka magaribi.

32 Ikiwa muzoga wa viumbe hao unaangukia kitu chochote, kikuwe ni kifaa cha mbao au nguo au ngozi au gunia au chombo chochote kinachotumiwa kwa kazi yoyote, chombo hicho kitakuwa kichafu mpaka magaribi. Kwa kukifanya kikuwe safi kinapaswa kusafishwa kwa maji.

33 Ikiwa muzoga wake umeangukia chombo cha udongo, basi, kitu chochote kilicho ndani ya chombo hicho ni kichafu na chombo hicho kinapaswa kuvunjwa.

34 Chakula au kinywaji chochote kilichokuwa ndani ya chombo hicho kitakuwa kichafu.

35 Kila kitu ambacho sehemu ya muzoga imekiangukia, kitakuwa kichafu. Ikiwa ni furu au jiko, kinapaswa kuvunjwa. Vitakuwa vichafu navyo ni vichafu kwenu.

36 Hata hivyo, kisima au chemichemi ya maji vitakuwa safi. Lakini kitu chochote kinachogusa muzoga kitakuwa kichafu.

37 Ikiwa sehemu ya muzoga inaangukia mbegu za kupanda, mbegu hizo hazitakuwa chafu.

38 Lakini ikiwa mbegu zimetiwa katika maji kwa kuota na sehemu yoyote ya muzoga ikaziangukia, basi, mbegu hizo ni chafu kwenu.

39 Ikiwa nyama yeyote munayeruhusiwa kula, anakufa mwenyewe, yeyote atakayegusa muzoga wake, atakuwa muchafu mpaka magaribi.

40 Mutu yeyote akikula nyama ya muzoga huo atafua nguo yake na atakuwa muchafu mpaka magaribi. Na yeyote atakayebeba muzoga huo, atafua nguo zake, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.

41 Kiumbe chochote kinachotambaa katika dunia ni chukizo kwenu, musikikule.

42 Chochote kinachotambaa kwa tumbo lake, chochote kinachotembea kwa miguu mine au miguu mingi, musikikule kwa maana ni chukizo.

43 Hivyo musijifanye kuwa chukizo kwa kula viumbe vinavyotambaa na hivyo kujichafua navyo.

44 Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.

45 Kwa sababu ni mimi Yawe niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu; kwa hiyo mukuwe watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu.

46 Hiyo basi, ndiyo sheria kuelekea nyama, ndege na viumbe vyote vyenye uzima ambavyo vinaishi ndani ya maji na inchi kavu,

47 kwa kutia tofauti kati ya kisichokuwa kichafu na kinachokuwa kichafu, kinachoweza kukuliwa na kisichoweza kukuliwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ