Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Ufunuo 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Muhuri wa saba

1 Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa saba, kukakuwa kimya mbinguni kwa muda wa nusu ya saa.

2 Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.

3 Kisha malaika mwingine akakuja kusimama karibu na mazabahu. Alikuwa akishika chetezo cha zahabu. Naye akapewa ubani mwingi kusudi autoe sadaka pamoja na maombi ya watu wote wa Mungu juu ya mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya kiti cha kifalme.

4 Moshi wa ule ubani pamoja na maombi ya watakatifu vilipanda mbele ya Mungu toka katika mukono wa yule malaika.

5 Kisha yule malaika akatwaa kile chetezo, akakijaza makaa ya moto toka kwenye mazabahu na kukitupa katika dunia. Na halafu kukakuwa ngurumo ya radi, makelele, umeme na tetemeko la inchi.


Wamalaika wanapiga baragumu

6 Wale wamalaika saba waliokuwa na baragumu saba wakajitayarisha kwa kuzipiga.

7 Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.

8 Kisha malaika wa pili akapiga baragumu. Halafu kitu kimoja chenye kufanana na mulima mukubwa unaowaka moto kikatupwa katika bahari, na sehemu moja ya tatu ya bahari ikageuka damu.

9 Sehemu moja ya tatu ya viumbe vinavyoishi katika bahari vikakufa, na sehemu moja ya tatu ya mashua ikaharibika.

10 Kisha malaika wa tatu akapiga baragumu. Halafu nyota kubwa iliyowaka kama mwenge, ikaanguka toka mbinguni na kujitupa juu ya sehemu moja ya tatu ya mito na juu ya chemichemi.

11 (Jina la ile nyota ni Uchungu.) Basi sehemu moja ya tatu ya maji ikakuwa uchungu, na watu wengi waliokunywa maji yale walikufa kwa sababu ya sumu iliyokuwa ndani yake.

12 Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.

13 Kisha nikaangalia tena, nami nikasikia tai mumoja akiruka juu sana katika anga akisema hivi kwa sauti kubwa: “Ole! Ole! Ole kwa wakaaji wa dunia, kutakaposikilika mulio wa zile baragumu zingine ambazo wamalaika watatu wanatayarisha kupiga!”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ