Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Mwanzo 7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mafuriko ya maji

1 Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.

2 Utwae pamoja nawe nyama wote wanaohesabiwa kuwa safi, dume saba na dike saba ya kila aina. Lakini nyama wanaohesabiwa kuwa wachafu, utwae dume na dike ya kila aina.

3 Vilevile utwae ndege dume saba na dike saba ya kila aina, kwa kulinda wazima aina zao katika dunia.

4 Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”

5 Noa akafanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru.

6 Noa alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati mafuriko ya maji yalipotokea juu ya inchi.

7 Noa, muke wake, wana wake na wake zao wakaingia ndani ya chombo kwa kuepuka mafuriko ya maji.

8 Nyama wanaohesabiwa kuwa safi, nyama wanaohesabiwa kuwa wachafu, ndege na viumbe vyote vinavyotambaa,

9 wawiliwawili, dume na dike, wakaingia ndani ya chombo pamoja na Noa kama vile Mungu alivyomwamuru.

10 Nyuma ya siku saba, maji ya mafuriko yakaanza kuifunika inchi.

11 Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita, katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemichemi zote za vilindi vya udongo zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.

12 Mvua ikanyesha juu ya inchi siku makumi ine, muchana na usiku.

13 Siku hiyohiyo mvua ilipoanza kunyesha, Noa, muke wake na wana wake, Semu, Hamu na Yafeti, pamoja na wake zao, wakaingia ndani ya chombo.

14 Waliingia wao wenyewe pamoja na aina zote za nyama wa pori, aina zote za nyama wanaofugwa, aina zote za nyama wanaotambaa na ndege wa kila aina.

15 Wawili wawili wa kila aina ya viumbe vyenye uzima waliingia ndani ya chombo pamoja na Noa.

16 Kila aina yao waliingia dume na dike kama vile Mungu alivyomwamuru Noa. Kisha, Yawe akafunga mulango wa chombo nyuma ya Noa.

17 Mafuriko yalidumu katika inchi kwa muda wa siku makumi ine. Maji yakaongezeka na kuiinua chombo, kikaelea juu ya udongo.

18 Maji yakaendelea kuongezeka zaidi juu ya inchi na chombo kikaelea juu yake.

19 Maji hayo yakakuwa mengi sana juu ya inchi, yakafunika milima yote mirefu katika inchi.

20 Yaliongezeka hata kufunika milima karibu metre saba na nusu.

21 Viumbe vyote vyenye uzima katika inchi vikakufa: ndege, nyama wa kufugwa, nyama wa pori, nyama wadogowadogo katika inchi kavu na wanadamu wote;

22 kila kiumbe chenye uzima katika inchi kavu kilikufa.

23 Mungu akaangamiza kila kiumbe kilichokuwa na pumzi ya uzima katika dunia: wanadamu, nyama, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Vyote viliangamizwa katika dunia. Noa tu ndiye aliyebaki na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo.

24 Maji hayo yalidumu katika inchi siku mia moja na makumi tano.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ