Mwanzo 36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Wazao wa Esau ( 1 Sik 1.34-37 ) 1 Hawa ndio wazao wa Esau ni kusema Edomu. 2 Esau alioa wake Wakanaa: Ada binti ya Eloni Muhiti, Oholibama binti ya Ana, binti ya Sibeoni Muhivi, 3 na Basemati binti ya Isimaeli, dada ya Nebayoti. 4 Ada alimuzalia Esau Elifazi, naye Basemati akamuzalia Reueli. 5 Oholibama alimuzalia Yeusi, Yalamu na Kora. Hao ndio wana wa Esau ambao wake zake walimuzalia alipokaa katika inchi ya Kanana. 6 Kisha, Esau akawatwaa wake zake, watoto wake wanaume na wanawake, watu wote wa nyumba yake, ngombe wake, nyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata katika inchi ya Kanana, akahamia pahali pengine, mbali na ndugu yake Yakobo. 7 Alifanya hivyo kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi hata wasiweze kuishi pamoja. Inchi walimokaa kama wageni haikuweza kuwatoshelea kwa sababu ya wingi wa nyama wao. 8 Kwa hiyo, Esau akakwenda kukaa katika inchi ya milima ya Seiri. Jina lingine la Esau ni Edomu. 9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba ya Waedomu katika inchi ya milima ya Seiri. 10 Wana wa Esau walikuwa Elifazi aliyezaliwa na Ada muke wake, na Reueli aliyezaliwa na Basemati muke wake mwingine. 11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi. 12 Elifazi alikuwa na habara, jina lake Timuna. Huyu alimuzalia mwana, jina lake Amaleki. 13 Basemati, muke wa Esau, alizaa Reueli. Wana wa Reueli walikuwa Nahati, Zera, Sama na Miza. 14 Oholibama, binti ya Ana, binti ya Sibeoni, alimuzalia Esau mume wake wana watatu: Yeusi, Yalamu na Kora. 15 Hawa ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Esau. Elifazi, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa Esau alizaa Temani, Omari, Sefo, Kenazi, 16 Kora, Gatamu na Amaleki. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Elifazi katika inchi ya Edomu, waliotokana na Ada, muke wa Esau. 17 Reueli mwana wa Esau, alizaa Nahati, Zera, Sama na Miza. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Reueli katika inchi ya Edomu, waliotokana na Basemati, muke wa Esau. 18 Wana wa Oholibama, muke wa Esau, walikuwa Yeusi, Yalamu na Kora. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Oholibama, binti ya Ana, muke wa Esau. 19 Basi, hao ndio wazao wa Esau, maana yake Edomu. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Wazao wa Seiri ( 1 Sik 1.38-42 ) 20 Hawa ndio wazao wa Seiri, Muhori, na ndio wenyeji wa inchi hiyo: Lotani, Sobali, Sibeoni, Ana, 21 Disoni, Eseri na Disani; kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake kati ya Wahori wa uzao wa Seiri, katika inchi ya Edomu. 22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani; na dada ya Lotani aliitwa Timuna. 23 Wana wa Sobali walikuwa Alwani, Manahati, Ebali, Sefo na Onamu. 24 Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana. Ana ndiye aliyeona chemichemi za maji ya moto katika jangwa, alipokuwa anachunga punda wa baba yake Sibeoni. 25 Watoto wa Ana walikuwa Disoni na binti mumoja jina lake Oholibama. 26 Wana wa Disoni walikuwa Hemudani, Esibani, Itirani na Kerani. 27 Wana wa Eseri walikuwa Bilihani, Zawani, na Akani. 28 Wana wa Disani walikuwa Usi na Arani. 29 Basi, hao ndio wakubwa wa Wahori: Lotani, Sobali, Sibeoni, Ana, 30 Disoni, Eseri na Disani; kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake katika inchi ya Seiri. Wafalme wa inchi ya Edomu ( 1 Sik 1.43-54 ) 31 Hawa ndio wafalme waliotawala katika inchi ya Edomu, mbele mufalme yeyote hajawatawala Waisraeli: 32 Bela mwana wa Beori alitawala inchi ya Edomu akiwa na makao yake makubwa katika muji wa Dinihaba. 33 Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosira akatawala pahali pake. 34 Yobabu alipokufa, Husamu wa inchi ya Watemani, akatawala pahali pake. 35 Husamu alipokufa, Hadadi mwana wa Bedadi akatawala pahali pake, makao yake makubwa yakiwa katika muji wa Awiti. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika inchi ya Moabu. 36 Hadadi alipokufa, Samula kutoka Masireka, akatawala pahali pake. 37 Samula alipokufa, Sauli kutoka Rehoboti, muji unaokuwa karibu na muto Furati, akatawala pahali pake. 38 Sauli alipokufa, Bali-Hanani mwana wa Akibori, akatawala pahali pake. 39 Bali-Hanani mwana wa Akibori alipokufa, Hadari akatawala pahali pake, na jina la muji wake likiwa Pau. Muke wa Akibori alikuwa Mehetabeli, binti ya Matiredi, binti ya Mezahaba. 40 Wakubwa wa makabila yaliyotokana na Esau kadiri ya makabila yao na makao yao walikuwa: Timuna, Alwa, Yeteti, 41 Oholibama, Ela, Pinoni, 42 Kenazi, Temani, Mibusari, 43 Magdieli na Iramu. Hao ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Edomu, maana yake, Esau, baba ya Edomu. Wametajwa kulingana na makao yao katika sehemu za inchi walizorizi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo