Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Mezali 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maonyo juu ya uasherati

1 Mwana wangu, sikia hekima yangu, tega sikio usikie elimu yangu.

2 Kwa hiyo, utaweza kulinda akili, na kinywa chako kitashika maarifa.

3 Midomo ya mwanamuke mupotovu ni mitamu kama asali, maneno yake ni laini kuliko mafuta;

4 lakini kwa mwisho ni michungu kama nyongo, ni mikali kama upanga wenye makali ngambo mbili.

5 Miguu yake inaelekea chini kwenye kifo, hatua zake zinaenda kuzimu.

6 Yeye haijali njia ya uzima, njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.

7 Sasa enyi wana wangu, musikilize, wala musisahau maneno ya kinywa changu.

8 Uepushe njia yako mbali naye, wala usiukaribie mulango wa nyumba yake,

9 kusudi usiwape wengine heshima yako, na watenda mabaya miaka yako,

10 wageni wasipate kushibishwa kwa mali yako, na faida ya kazi yako kuishia katika nyumba ya mugeni.

11 Kwa mwisho wa maisha yako utaomboleza, wakati mwili wako utakapoangamizwa.

12 Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?

13 Sikusikiliza sauti ya walimu wangu, wala kuwategea sikio wale walionifundisha.

14 Nikakuwa karibu ya kuangamia kabisa katika kusanyiko na mukutano wa watu.”

15 Kunywa maji ya birika lako mwenyewe, maji yanayobubujika katika kisima chako mwenyewe.

16 Kwa nini chemichemi zako zitawanywe mbali, na vijito vya maji katika barabara?

17 Hiyo ni yako wewe mwenyewe, wala usiwashirikishe watu wengine.

18 Chemichemi yako ibarikiwe, umufurahie muke uliyemwoa ukiwa kijana.

19 Ni muzuri kama pongo, anapendeza kama paa. Mapenzi yake yakufurahishe kila wakati, uvutwe siku zote na mapendo yake.

20 Mwana wangu, kwa nini kutekwa na mwanamuke mwasherati? Kwa nini kukumbatia mwanamuke mugeni katika kifua?

21 Maana mwenendo wa kila mutu ni wazi mbele ya Yawe; yeye anachunguza njia zake zote.

22 Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.

23 Yeye anakufa kwa ajili ya ukosefu wa mafundisho, anaangamia kwa sababu ya upumbafu wake mukubwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ