Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Matayo 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Yesu anaponyesha mwenye ukoma
( Mk 1.40-45 ; Lk 5.12-16 )

1 Yesu aliposhuka toka kwa mulima, makundi mengi ya watu wakamufuata.

2 Halafu mutu mumoja mwenye ukoma akakuja, akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”

3 Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.

4 Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Yesu anaponyesha mutumishi wa mukubwa wa waaskari
( Lk 7.1-10 )

5 Yesu alipokuwa akiingia katika muji Kapernaumu, mukubwa mumoja wa waaskari akamufikia na kumusihi,

6 akisema: “Bwana, mutumishi wangu anawezwa na ugonjwa wa kupooza, naye amelala ndani ya nyumba, akiteswa sana.”

7 Yesu akamwambia: “Nitakuja kumuponyesha.”

8 Lakini yule mukubwa akamujibu: “Bwana, mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu. Lakini uamuru kwa neno tu na mutumishi wangu atapona.

9 Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena nina waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’, naye anakwenda. Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’, naye anakuja. Na nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’, naye anafanya vile.”

10 Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.

11 Ninawaambia wazi kwamba watu wengi watakuja toka mashariki na magaribi, nao watachangia meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwenye karamu katika Ufalme wa mbinguni.

12 Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”

13 Kisha Yesu akamwambia yule mukubwa wa waaskari hivi: “Urudie kwako, na ifanyike kwako sawa ulivyoamini.” Na saa ile ile mutumishi wake akapona.


Yesu anaponyesha wagonjwa wengi
( Mk 1.29-34 ; Lk 4.38-41 )

14 Kisha Yesu akafika kwa nyumba ya Petro, na mule akamukuta mama mukwe wa Petro amelala katika kitanda na ugonjwa wa homa.

15 Yesu akamugusa mukono, naye akapona homa. Halafu mama yule akasimama na kuanza kumushugulikia.

16 Na ilipokuwa magaribi, wakamuletea Yesu watu wengi waliokuwa na pepo. Naye akawafukuza wale pepo akiwaamuru kwa neno tu na kuwaponyesha wagonjwa wote.

17 Alifanya hivi kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Isaya: “Yeye alitwaa uzaifu wetu, naye amebeba muzigo wa magonjwa yetu.”


Namna ya kumufuata Yesu
( Lk 9.57-62 )

18 Yesu alipoona kundi la watu wakimuzunguka, akatoa amri ya kuvuka ngambo ingine ya ziwa.

19 Mwalimu mumoja wa Sheria akamufikia na kumwambia: “Mwalimu, nitakufuata popote utakapokwenda.”

20 Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”

21 Na mutu mwingine mumoja kati ya wanafunzi wake akamwambia: “Bwana, unipe ruhusa kwanza niende kuzika baba yangu.”

22 Lakini Yesu akamujibu: “Unifuate mimi, uwaache hao wafu wazike wafu wao.”


Yesu anatuliza zoruba
( Mk 4.35-41 ; Lk 8.22-25 )

23 Halafu Yesu akaingia ndani ya chombo, nao wanafunzi wake wakaenda naye.

24 Mara moja zoruba kubwa ikatokea katika ziwa na maji yakajitupatupa ndani ya chombo. Lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.

25 Wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha na kumwambia: “Bwana, utuokoe! Tunakufa!”

26 Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.

27 Nao wakashangaa, wakisema: “Huyu ni mutu gani, hata zoruba na ziwa vinamutii?”


Yesu anaponyesha watu wawili wenye pepo
( Mk 5.1-20 ; Lk 8.26-39 )

28 Yesu alipofika ngambo ingine ya ziwa la Galilaya, katika inchi ya Wagedari, watu wawili wenye pepo wakamufikia, wakitoka kwenye makaburi. Watu wale walikuwa na pepo wakali sana, hata hakuna mutu aliyesubutu kupita katika njia ile.

29 Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”

30 Na karibu na pale kulikuwa kundi kubwa la nguruwe wakijitafutia chakula.

31 Wale pepo wakamusihi Yesu wakisema: “Ikiwa unataka kutufukuza, ututume tuingie ndani ya wale nguruwe.”

32 Na Yesu akawaambia: “Mwende!” Basi wakatoka ndani ya wale watu na kuingia ndani ya nguruwe. Mara moja kundi zima likatelemuka mbio toka kwenye maporomoko ya mulima na kujitupa ndani ya ziwa nao wakazama ndani ya maji.

33 Wachungaji wa nguruwe wale wakaenda mbio katika muji kupasha habari za mambo yaliyotendeka na habari ya wale watu wawili waliokuwa na pepo.

34 Basi watu wote wa muji wakatoka kwa kumufikia Yesu na wakati walipomwona wakamusihi aondoke katika inchi yao.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ