Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Luka 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mamlaka ya Yesu yanatoka wapi?
( Mat 21.23-27 ; Mk 11.27-33 )

1 Siku moja Yesu alikuwa katika hekalu akiwafundisha watu na kuhubiri Habari Njema. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza:

2 “Utuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya, na ni nani aliyekupa mamlaka yale?”

3 Yesu akawajibu: “Mimi vilevile nitawauliza ulizo hili moja. Muniambie,

4 Yoane alipata mamlaka ya kubatiza kutoka kwa nani? Kwa Mungu au kwa watu?”

5 Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atauliza: ‘Kwa sababu gani basi hamukumwaminia?’

6 Lakini vilevile hatuwezi kusema kwamba yalitoka kwa watu, kwa maana watu wote watatutupia mawe, kwa sababu wanasadiki kwamba Yoane alikuwa nabii.”

7 Basi wakajibu kwamba hawajui mamlaka yake yalitoka wapi.

8 Yesu akawaambia: “Nami vilevile sitawaambia ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”


Mufano wa walimaji wabaya
( Mat 21.33-46 ; Mk 12.1-12 )

9 Akaendelea kuwaambia watu mufano huu: “Mutu mumoja alipanda shamba la mizabibu. Kisha kupatana kugawanyana mavuno na walimaji wamoja watakaobaki wakitunza shamba lake, akaenda safari katika inchi ingine na kukaa kule kwa muda murefu.

10 Siku za mavuno zilipotimia, akamutuma mutumishi wake mumoja kwa wale walimaji kusudi wamupatie sehemu yake ya mavuno. Lakini wale walimaji wakamupiga na kumurudisha mikono mitupu.

11 Mwenye shamba akatuma tena kwao mutumishi mwingine, lakini wakamupiga vilevile na kumutukana. Kisha wakamurudisha mikono mitupu.

12 Mwenye shamba akatuma tena kwao mutumishi wa tatu, yule naye wakamwumiza na kumutupa inje ya shamba.

13 Halafu yule mwenye shamba akasema: ‘Nitafanya nini? Nitamutuma mwana wangu mupendwa; labda watamuheshimu.’

14 Lakini wale walimaji walipomwona akikuja, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue kusudi shamba hili lipate kuwa urizi wetu.’

15 Halafu wakamukamata wakamwua na kutupa maiti yake inje ya shamba.” Kisha Yesu akauliza: “Basi yule mwenye shamba atawatendea walimaji wale namna gani?

16 Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”

17 Lakini Yesu akawaangalia na kuwauliza: “Maana ya Maandiko haya Matakatifu ni gani? ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.’

18 Kila mutu atakayeanguka juu ya jiwe lile, atavunjika na yule litakayemwangukia, litamuponda.”


Ulizo juu ya kulipa kodi
( Mat 22.15-22 ; Mk 12.13-17 )

19 Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.

20 Basi wakaanza kumuvizia Yesu, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa kama watu wazuri kusudi wamunase katika masemi. Na kwa njia ile waweze kumutoa katika mikono ya watawala wa inchi.

21 Wale wapelelezi wakamwuliza: “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha maneno ya kweli. Vilevile wewe hauangalii cheo cha mutu, lakini unafundisha juu ya namna ya kuishi ambayo Mungu anaamuru kufuata.

22 Utuambie basi, Sheria inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana?”

23 Lakini kwa kuwa Yesu alitambua udanganyifu wao, akawaambia:

24 “Munionyeshe kikoroti kimoja cha feza.” Kisha akawauliza: “Sura hii na jina hili linaloandikwa hapa ni vya nani?” Nao wakajibu: “Ni vya Mufalme wa Roma.”

25 Halafu Yesu akawaambia: “Basi mumupe Mufalme wa Roma vinavyokuwa vyake, na Mungu vinavyokuwa vyake.”

26 Basi watu wale hawakuweza kumunasa katika neno lolote mbele ya watu, lakini wakashangaa na jibu lake, nao wakanyamaza.


Ulizo juu ya ufufuko
( Mat 22.23-33 ; Mk 12.18-27 )

27 Wasadukayo wamoja (ndio wale watu wanaosema kwamba wafu hawatafufuka) wakamufikia Yesu na kumwuliza:

28 “Mwalimu, Musa alituamuru: Mutu akiwa na ndugu yake, naye akikufa na kuacha muke wake bila mutoto, yule ndugu yake anapaswa kumwoa yule mujane na kumuzalia ndugu yake marehemu watoto.

29 Basi kulikuwa wandugu saba. Wa kwanza alioa mwanamuke, lakini mutu yule akakufa bila kuacha mutoto.

30 Ndugu wa pili akaoa yule mujane, akakufa vilevile bila kuacha mutoto.

31 Na ikakuwa vile kwa ndugu wa tatu na hata kwa wote saba. Wote wakakufa bila kuacha mutoto.

32 Na kwa mwisho, yule mwanamuke akakufa vilevile.

33 Sasa, siku wafu watakapofufuka, muke yule atakuwa wa nani, kwa maana wote saba walikuwa wamemwoa?”

34 Yesu akawajibu: “Watu wa nyakati hizi wanaoa na kuolewa.

35 Lakini wale watakaohesabiwa kwamba wanastahili kufufuliwa na kuishi katika nyakati zile zitakazokuja, hawataoa wala kuolewa.

36 Na zaidi ya ile hawataweza kufa tena, kwa sababu wataishi sawa vile wamalaika wanavyoishi. Nao watakuwa watoto wa Mungu, kwa sababu wamefufuliwa.

37 Musa alionyesha waziwazi kwamba wafu watafufuka. Katika maandiko yake yanayosema juu ya kichaka kilichowaka moto, yeye anamutaja Bwana kuwa ni ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’

38 Yeye si Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wanaokuwa wazima; maana mbele yake wote wanaishi.”

39 Walimu wamoja wa Sheria wakasema: “Mwalimu, umejibu vizuri!”

40 Na hakuna mutu aliyesubutu tena kumwuliza maneno mengine.


Ulizo juu ya Mwana wa Daudi
( Mat 22.41-46 ; Mk 12.35-37 )

41 Yesu akaongeza kuwaambia: “Namna gani wanaweza kusema kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?

42 Daudi yeye mwenyewe alisema katika kitabu cha Zaburi: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu

43 mpaka nitakapoweka waadui zako chini ya miguu yako.’

44 Daudi anamwita Kristo ‘Bwana’; namna gani basi Kristo anaweza kuwa Mwana wake?”


Maonyo juu ya walimu wa Sheria
( Mat 23.1-36 ; Mk 12.38-40 )

45 Watu wote walipokuwa wakimusikiliza Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:

46 “Mujiepushe na walimu wa Sheria wanaopenda kujitembeza, wakivaa kanzu ndefu na kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano. Wanapenda vilevile kuikaa katika viti vya mbele ndani ya nyumba za kuabudia, na kwenye nafasi za heshima katika karamu.

47 Wananyanganya mali ya wajane na kuomba maombi marefu kusudi waonekane mbele ya watu. Kwa sababu hii watahukumiwa vikali sana!”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ