Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Kutoka 31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Wafundi wa kutayarisha hema la mukutano
( Kut 35.30–36.1 )

1 Yawe akamwambia Musa:

2 Mimi nimemuchagua Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, wa kabila la Yuda

3 na kumujaza Roho wangu. Nimemupatia ufahamu na akili, maarifa na ufundi,

4 kusudi afanye kazi za ufundi na kufanya kazi za kufua zahabu, feza na shaba.

5 Nimemupatia ujuzi wa kuchonga mawe ya kupamba, kuchonga mbao, na ujuzi wa kila aina ya ufundi.

6 Vilevile nimemuchagua Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, afanye kazi pamoja naye. Vilevile nimewapa uwezo mukubwa watu wengine kwa ajili ya kazi mbalimbali, kusudi watengeneze vifaa vyote nilivyoagiza vifanywe:

7 hema la mukutano, Sanduku la Agano na kiti cha ushuhuda juu yake, pamoja na vifaa vyake vyote,

8 meza na vyombo vyake, kinara safi cha taa na vyombo vyake, mazabahu ya kufukizia ubani,

9 mazabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika la maji pamoja na tako lake,

10 nguo takatifu ya kuhani Haruni na wana wake ambao watafanya kazi ya ukuhani,

11 mafuta ya kupakaa na ubani wenye harufu nzuri kwa ajili ya Pahali Patakatifu. Vitu hivyo vyote vitatengenezwa kulingana kabisa na jinsi nilivyokuamuru.


Sabato: siku ya kupumzika

12 Yawe akamwambia Musa:

13 Uwaambie Waisraeli hivi: Ninyi mutashika hakika Sabato zangu, kwa sababu hizo ni kitambulisho kati yenu na mimi kwa vizazi vyote kwamba mimi ndimi ninayewatakasa.

14 Mutashika Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeichafua siku hiyo anapaswa kuuawa. Na mutu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake.

15 Mutafanya kazi zenu kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba ni siku ya Sabato, ni siku ya kupumzika ambayo ni takatifu kwa ajili ya Yawe. Mutu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo lazima atauawa.

16 Kwa hiyo Waisraeli watashika Sabato katika vizazi vyao vyote kama vile kitambulisho cha agano la milele.

17 Jambo hili litakuwa kitambulisho cha kudumu kati ya Waisraeli na mimi, maana mimi Yawe nilifanya mbingu na dunia kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba niliacha kufanya kazi, nikapumzika.

18 Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ