Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Kutoka 22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maagizo juu ya malipo

1 Mwizi akikamatwa yuko anavunja nyumba, naye akipigwa na kufa, aliyemwua hana kosa la mauaji.

2 Lakini mwizi akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemwua atakuwa na kosa. Mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzishwa kwa kulipa kile alichoiba.

3 Kama nyama aliyeibwa, akuwe ni ngombe, punda au kondoo, akipatikana muzima kwa mwizi, basi, yule mwizi atalipa nyama wawili.

4 Mutu akiwakulishia nyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachilia nyama wake kula katika shamba la mutu mwingine, atalipa hasara ile kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.

5 Mutu akiwasha moto nao ukichoma miti ya miiba na kusambaa mpaka kuteketeza miganda ya ngano au ngano ya mutu mwingine ambayo bado haijavunwa au shamba lote likiteketea, aliyewasha moto ule anapaswa kulipa hasara ile yote.

6 Mutu akimwachia mwenzake feza au mali nyingine amutunzie, kisha ikaibiwa ndani ya nyumba yake, mwizi akipatikana anapaswa kulipa bei yake mara mbili.

7 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atakaribia mbele ya Mungu kwa kuhakikisha kwamba yeye hakuiba mali ya mwenzake.

8 Kukitokea ubishi juu ya ngombe, au punda, au kondoo, au nguo, au kitu chochote kilichopotea ambacho kila mumoja anadai kwamba ni chake, wale wanaobishana wataletwa mbele ya Mungu. Yule ambaye Mungu ataamua kwamba amekosa, atamulipa mwenzake mara mbili.

9 Mutu akimupatia mwenzake punda, ngombe, kondoo au nyama mwingine yeyote amutunzie na nyama yule akikufa au akipelekwa bila mutu yeyote kushuhudia,

10 kiapo mbele ya Yawe kitaamua kati yao, kwa kuonyesha kwamba yule aliyepewa hakuiba mali ya mwenzake. Mwenye nyama yule atakubali kile kiapo na yule mwenzake hatalipa malipo yoyote.

11 Lakini kama aliibiwa kwake, anapaswa kumulipa mwenye naye.

12 Kama yule nyama aliraruliwa na nyama wa pori, yule mutu aliyekuwa amepewa anapaswa kumuleta kama ushuhuda. Hatalipa malipo yoyote kwa ajili ya nyama aliyeraruliwa na nyama wa pori.

13 Mutu akiazima nyama kwa mwenzake, kisha nyama yule akaumia au akakufa wakati mwenye naye hayuko, aliyeazima nyama yule anapaswa kumulipa kwa ukamilifu.

14 Lakini kama mwenye naye alikuwa pale, basi aliyemwazima hatalipa kitu chochote. Kama alikuwa ni nyama aliyeazimwa, mwenye naye atakubali tu bei ya kuazima.


Sheria za namna ya kuishi

15 Mutu akimutongoza binti ambaye hajachumbiwa, akilala naye, hakika atalipa mali na kumwoa binti yule.

16 Baba wa yule binti akikataa kabisa kumwoesha binti yake, mutu yule atalipa feza ya mali inayostahili binti anayekuwa bikira.

17 Usimwache mwanamuke muchawi aishi.

18 Anayezini na nyama hakika atauawa.

19 Anayemutolea mungu mwingine sadaka pahali pa Yawe pekee, lazima aangamizwe kabisa.

20 Musimwonelee mugeni wala kumutesa, maana nanyi vilevile mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.

21 Musimutese mujane au yatima.

22 Kama mukiwatesa wale, nao wakinililia, hakika nitakisikiliza kilio chao,

23 na hasira yangu itawaka, nami nitawaua ninyi kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu wayatima.

24 Ukimukopesha feza mutu yeyote kati ya watu wangu wanaokuwa wamasikini, usikuwe kwake kama mudai, wala usimulipishe faida.

25 Ukitwaa nguo ya mwenzako kama rehani, lazima umurudishie mbele ya jua kutua,

26 kwa sababu hiyo ndiyo nguo yake ya pekee; ndiyo atakayojifunika nayo. Au unazani atalalia nini? Akinililia nitamusikiliza, maana mimi ni mwenye huruma.

27 Usimutukane Mungu, wala kumulaani mukubwa wa watu wako.

28 Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.

29 Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.

30 Ninyi mutakuwa watu waliotakaswa kwa ajili yangu. Kwa hiyo hamutakula nyama ya nyama aliyeuawa na nyama wa pori. Nyama hiyo mutaitupia imbwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ