Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Kutoka 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Amri kumi
( Kumb 5.1-21 )

1 Mungu alisema maneno haya yote:

2 Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.

3 Usikuwe na miungu mingine isipokuwa mimi.

4 Usijifanyie sanamu ya miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.

5 Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.

6 Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.

7 Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.

8 Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato.

9 Siku sita fanya kazi na tenda mambo yako yote.

10 Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala nyama wako wa kufugwa, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako.

11 Maana kwa siku sita mimi Yawe niliumba mbingu na inchi, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Yawe nilibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.

12 Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.

13 Usiue.

14 Usizini.

15 Usiibe.

16 Usimushuhudie mwenzako uongo.

17 Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.

18 Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,

19 wakamwambia Musa: Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini Yawe asiseme nasi, tusikufe.

20 Musa akawaambia: Musiogope, maana Mungu amekuja kuwapima kusudi mupate kumwogopa siku zote na musitende zambi.

21 Watu wote wakasimama mbali wakati Musa alipokaribia lile wingu zito Mungu alimokuwa.

22 Yawe akamwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.

23 Mutaniheshimu mimi peke yangu wala musijifanyie miungu ya feza wala ya zahabu.

24 Ninyi mutanijengea mazabahu ya udongo. Juu yake mutanitolea kondoo wenu na ngombe wenu kama sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Pahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, pale pale mimi mwenyewe nitawafikia na kuwabariki.

25 Kama mukinijengea mazabahu ya mawe, musiitengeneze kwa mawe ya kuchonga, maana mukitumia vyombo vya kuchonga mawe, mutaichafua.

26 Wala musitengeneze mazabahu yenye ngazi za kupandia, mutu asipate kuona uchi wa yule anayepanda juu yake.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ