Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Kutoka 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mutoto Musa anaokotwa katika muto Nili

1 Kulikuwa mutu mumoja wa ukoo wa Walawi aliyemuoa mwanamuke mumoja ambaye vilevile alikuwa wa ukoo wa Walawi.

2 Basi, mwanamuke yule akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Alipoona kwamba mutoto yule muchanga alikuwa muzuri, akamuficha kwa muda wa miezi mitatu.

3 Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo, akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani.

4 Dada ya yule mutoto akajificha karibu na pahali pale kusudi aone yatakayomupata ndugu yake.

5 Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae.

6 Alipokifungua, akamwona yule mutoto muchanga akilia. Basi, akamwonea huruma, akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.”

7 Palepale dada ya yule mutoto akajitokeza, akamwambia binti ya mufalme: “Niende nikutafutie yaya kati ya wanawake Waebrania akulelee mutoto huyu?”

8 Binti ya mufalme akamwambia: “Kwenda.” Basi, yule binti akaenda, akamwita mama ya yule mutoto.

9 Binti ya mufalme akamwambia yule mama: “Utunze mutoto huyu, umulee kwa ajili yangu, nami nitakulipa mushahara wako.” Basi, yule mama akamutwaa mutoto, akamulea.

10 Mutoto alipokuwa mukubwa, mama yake akamupeleka kwa binti ya mufalme, naye akamutwaa na kumufanya mwana wake. Binti ya mufalme akasema: “Nimemutoa ndani ya maji,” kwa hiyo akamupa mutoto yule jina Musa.


Musa anakimbilia Midiani

11 Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.

12 Musa akaangalia huku na huko na alipoona kwamba hakuna mutu karibu, akamwua yule Mumisri na kumuficha ndani ya muchanga.

13 Kesho yake, Musa akatoka tena, akaona Waebrania wawili wakipigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosa: “Kwa nini unamupiga mwenzako?”

14 Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?” Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!”

15 Naye mufalme wa Misri aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumwua Musa. Lakini Musa akamukimbia mufalme, akaenda kukaa katika inchi ya Midiani. Siku moja, Musa alikuwa akikaa kando ya kisima cha maji.

16 Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao.

17 Wachungaji wengine wakakuja na kuwafukuza wale wabinti. Lakini Musa akawasaidia wabinti wale na kuwakunywesha nyama wao.

18 Walipomurudilia baba yao Rueli, yeye akawauliza: “Mbona leo mumerudi upesi hivyo?”

19 Nao wakamujibu: “Mumisri mumoja alituokoa toka mikono ya wale wachungaji, naye mwenyewe akachota maji na kuwakunywesha nyama wetu.”

20 Baba yao akawauliza wabinti zake: “Yuko wapi? Mbona mumemwacha kule? Mumwite akuje akule chakula.”

21 Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake.

22 Zipora akamuzalia mutoto mwanaume. Musa akasema: “Nimekimbilia katika inchi ya kigeni”, kwa hiyo akamupa yule mutoto jina Gersomi.


Kilio cha Waisraeli katika utumwa

23 Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.

24 Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.

25 Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ