Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Isaya 23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maangamizi ya Tiro na Sidona

1 Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro. Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi. Kivuko na muji wenu vimeharibiwa. Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.

2 Munyamaze kwa mushangao, enyi wakaaji wa visanga, mutulie enyi wachuuzi wa Sidona. Wajumbe wenu walipita katika bahari kubwakubwa,

3 walisafiri katika bahari nyingi. Mapato yenu yalikuwa ngano ya Misri, mukaweza kufanya biashara na mataifa.

4 Umefezeheka, ewe Sidona, muji wenye upango kandokando ya bahari! Bahari yenyewe inatangaza: Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa, wala sijazaa; sikulea vijana wanaume, wala kukomalisha wabinti!

5 Habari zitakapoifikia Misri kwamba Tiro imeangamizwa, Wamisri watafazaika sana.

6 Muomboleze enyi wenyeji wa Foinike! Mujaribu kukimbilia Tarsisi.

7 Basi, huu ndio muji wa furaha wa Tiro, muji ambao ulijengwa zamani za kale, ambao wakaaji wake walikwenda kurizi inchi za mbali?

8 Ni nani aliyepanga mambo haya juu ya Tiro, muji uliosimika wafalme, wachuuzi wake walikuwa wakubwa, wakaheshimiwa katika dunia yote?

9 Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.

10 Mulime sasa udongo wenu, enyi wakaaji wa Tarsisi; maana hamuna tena kivuko kwa ajili ya mashua kubwa.

11 Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.

12 Alisema: Ewe binti Sidona, hautaweza kufanya sherehe tena; hata ukikimbilia Kipuro, kule nako hautapata pumziko!

13 (Ni Wakaldea, wala si Waasuria, waliowaacha nyama wa pori waushambulie muji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia muji huo minara ya kuushambulia, wakabomoa nyumba zake na kuufanya mabomoko.)

14 Mulie enyi mashua za Tarsisi, maana kimbilio lenu limeharibiwa.

15 Hapo muji wa Tiro utasahauliwa kwa muda wa miaka makumi saba, muda wa maisha ya mufalme. Kisha miaka hiyo makumi saba, muji wa Tiro utapatwa na kile watu wanachoimba juu ya kahaba:

16 Kamata kinubi chako uzungukezunguke ndani ya muji, ewe kahaba uliyesahauliwa! Imba nyimbo tamutamu. Imba nyimbo nyinginyingi, kusudi upate kukumbukwa tena.

17 Kisha miaka hiyo makumi saba, Yawe atauazibu muji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuzisha kwa mataifa yote ya dunia.

18 Feza utakayopata itatakaswa kwa ajili ya Yawe. Hawatalinda feza hiyo lakini wale wanaomwabudu Yawe wataitumia kwa kununua chakula kingi na nguo nzuri.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ