Isaya 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Wimbo wa shukrani 1 Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji. 2 Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. 3 Mutachota maji kwa furaha kutoka visima vya wokovu. 4 Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa. 5 Mumwimbie Yawe sifa maana ametenda mambo makubwa; haya yajulikane katika dunia yote. 6 Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo