Hosea 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Hosea na mwanamuke muzinzi 1 Yawe akaniambia: Kwenda tena umupende mwanamuke anayependwa na mwanaume mwingine na ambaye ni muzinzi. Umupende kama vile mimi Yawe ninavyowapenda Waisraeli, ingawa wao wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu. 2 Basi, nikamupata huyo mwanamuke kwa vikoroti kumi na vitano vya feza na saki nyingi za shayiri. 3 Kisha nikamwambia: Unapaswa kuwa wangu kwa siku nyingi bila kufanya uzinzi au kuwa muke wa mutu mwingine; nami vilevile nitakuwa mwaminifu. 4 Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu. 5 Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo