Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Hosea 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hosea na mwanamuke muzinzi

1 Yawe akaniambia: Kwenda tena umupende mwanamuke anayependwa na mwanaume mwingine na ambaye ni muzinzi. Umupende kama vile mimi Yawe ninavyowapenda Waisraeli, ingawa wao wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.

2 Basi, nikamupata huyo mwanamuke kwa vikoroti kumi na vitano vya feza na saki nyingi za shayiri.

3 Kisha nikamwambia: Unapaswa kuwa wangu kwa siku nyingi bila kufanya uzinzi au kuwa muke wa mutu mwingine; nami vilevile nitakuwa mwaminifu.

4 Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.

5 Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ