Hosea 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo. Kumurudilia Mungu na hali mupya 2 Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu. 3 Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo. 4 Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma. 5 Yawe anasema: Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu; nitawapenda tena kwa moyo wangu wote, maana sitawakasirikia tena. 6 Nitakuwa kama umande kwa Waisraeli nao watachanua kama mayungiyungi, watakuwa na mizizi kama muti wa mwerezi wa Lebanoni. 7 Vichipukizi vyao vitazaa sana, uzuri wao utakuwa kama mizeituni, harufu yao nzuri kama maua ya Lebanoni. 8 Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni. 9 Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu. 10 Yeyote anayekuwa na hekima aelewe mambo haya, mutu anayekuwa na akili ayatambue. Maana njia za Yawe ni zenye kunyooka; watu wa haki wanazifuata, lakini wenye zambi wanaanguka katika njia hizo. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo