Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Hesabu 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuwekwa kwa taa

1 Yawe akamwambia Musa:

2 Umwambie Haruni kwamba wakati atakapoweka zile taa saba kwenye kinara, azipange kusudi ziangaze upande wa mbele wa kinara hicho.

3 Haruni akatii maagizo hayo, akaweka taa hizo kusudi ziangaze upande wa mbele wa kinara, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.

4 Toka sehemu za juu mpaka chini kinara hicho cha taa kilikuwa kimetengenezwa kwa ufundi mukubwa kwa zahabu iliyofuliwa kufuatana na mufano ambao Yawe alikuwa amemwonyesha Musa.


Kutakaswa kwa Walawi

5 Tena Yawe akamwambia Musa:

6 Uwatenge Walawi kutoka Waisraeli na kuwatakasa.

7 Hivi ndivyo utakavyowatakasa: uwanyunyizie maji ya utakaso kisha uwaambie wajinyoe mwili muzima, wafue nguo zao na kujitakasa.

8 Kisha watatwaa mwana-ngombe dume mumoja pamoja na sadaka yake ya vyakula, ni kusema unga laini uliochanganywa na mafuta; nawe utatwaa mwana-ngombe dume wingine kwa ajili ya zambi.

9 Kisha utawakusanya watu wote wa Israeli na kuwaleta Walawi mbele ya hema la mukutano.

10 Utakapowaleta Walawi mbele yangu, Waisraeli watawawekea Walawi mikono.

11 Halafu Haruni atawaweka hao mbele yangu kama sadaka ya kutikiswa kutoka kwa Waisraeli wanitumikie.

12 Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya ngombe dume hao; mumoja wao utamutoa kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, na huyo mwingine utamutoa kuwa sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwangu, kwa kuwafanyia Walawi upatanisho.

13 Kisha utawasimamisha Walawi mbele ya Haruni na wana wake na kuwaweka mbele yangu kama vile sadaka ya kutikiswa.

14 Hivi ndivyo utakavyowatenga Walawi kati ya Waisraeli wengine kusudi wakuwe wangu.

15 Kisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama vile sadaka ya kutikiswa wataingia kwa kutumika katika hema la mukutano.

16 Hao wametolewa wakuwe wangu kabisa, pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli.

17 Maana wazaliwa wote wa kwanza kati ya Waisraeli ni wangu, wanadamu na nyama; maana niliwatakasa kwa ajili yangu siku nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza katika inchi ya Misri.

18 Sasa ninawatwaa Walawi pahali pa wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli,

19 na nimewatoa kwa Haruni na wana wake, kama vile zawadi kutoka kwa Waisraeli, kusudi wafanye kazi katika hema la mukutano kwa ajili ya Waisraeli na kuwafanyia upatanisho kusudi kusitokee pigo kati ya Waisraeli wakikaribia Pahali Patakatifu.

20 Kwa hiyo Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja wakatakasa Walawi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.

21 Walawi wakajitakasa zambi na kufua nguo zao, naye Haruni akawatoa kama vile sadaka ya kutikiswa mbele ya Yawe. Vilevile, Haruni akafanya upatanisho kwa ajili yao kwa kuwatakasa.

22 Kisha hayo Walawi wakaingia na kufanya kazi yao katika hema la mukutano chini ya usimamizi wa Haruni na wana wake, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.

23 Yawe akamwambia Musa:

24 Kila Mulawi mwenye umri wa miaka makumi mbili na mitano na zaidi, atatumika katika hema la mukutano.

25 Na tangu umri wa miaka makumi tano ataacha kazi; asitumike tena.

26 Lakini, anaweza kuwasaidia Walawi wenzake wanapotumika katika hema, lakini haruhusiwi kufanya kazi yoyote peke yake. Ndivyo utakavyowapangia Walawi kazi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ