Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

Hesabu 34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mipaka ya inchi

1 Yawe akamwambia Musa:

2 Uwaamuru Waisraeli ukisema: Mutakapoingia Kanana, inchi ambayo ninawapa ikuwe inchi yenu, mipaka ya eneo lenu lote itakuwa kama hivi.

3 Upande wa kusini mupaka wenu utakuwa kutoka jangwa la Sini kupitia upande wa Edomu. Utaanzia mashariki upande wa kusini mwisho wa bahari ya Chumvi.

4 Kisha utapinda kusini kuelekea mupando wa Akarabimu na kupitia Sini mpaka Kadesi-Barnea, upande wa kusini. Kutoka pale, mupaka utapinda kuelekea kaskazini-magaribi mpaka Hasari-Adari na kupita mpaka Azimoni.

5 Kutoka Azimoni utapinda kuelekea kijito cha Misri kwenye mupaka wa Misri na kuishia bahari ya Mediteranea.

6 Mupaka wenu wa upande wa magaribi utakuwa bahari ya Mediteranea.

7 Mupaka wenu wa upande wa kaskazini utakuwa kama hivi: kutoka bahari ya Mediteranea, mpaka kwenye mulima Hori,

8 na kutoka mulima Hori, mpaka kwenye njia inayokwenda Hamati, na kuendelea mpaka Sedadi,

9 kupitia Zifuroni na kuishia Hazari-Enani. Huo utakuwa mupaka wenu wa kaskazini.

10 Mupaka wenu wa upande wa mashariki mutauweka kutoka Hazari-Enani mpaka Sefamu.

11 Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,

12 halafu utateremuka kufuata muto Yordani mpaka bahari ya Chumvi hii ndiyo itakuwa inchi yako kama vile mupaka unavyokuwa.

13 Basi, Musa akawaambia Waisraeli: Hii ndiyo inchi mutakayoirizi kwa kupiga kura, inchi ambayo Yawe ameagiza ipewe kwa makabila tisa na nusu.

14 Kabila la Rubeni na la Gadi, na nusu ya kabila la Manase yamepata urizi wao kulingana na ukoo zao.

15 Makabila hayo mawili na nusu yamepata urizi wao ngambo ya muto Yordani upande wa mashariki, kuelekea Yeriko, jua linakotokea.


Viongozi watakaosimamia mugawanyo wa inchi

16 Yawe akamwambia Musa:

17 Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni ndio watakaowagawanyia watu inchi kuwa mali yao.

18 Utatwaa vilevile kiongozi mumoja kutoka kila kabila kwa kusaidia katika ugawanyaji wa inchi.

19 Haya ndiyo majina yao: Kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.

20 Kabila la Simeoni, Semweli mwana wa Amihudi.

21 Kabila la Benjamina, Elidadi mwana wa Kisiloni.

22 Kabila la Dani, Buki mwana wa Yogli.

23 Kabila la Manase mwana wa Yosefu, Hanieli mwana wa Efodi.

24 Kabila la Efuraimu mwana wa Yosefu, Kemueli mwana wa Sifutani.

25 Kabila la Zebuluni, Elisafani mwana wa Parnaki.

26 Kabila la Isakari, Paltieli mwana wa Azani.

27 Kabila la Aseri, Ahihudi mwana wa Selomi

28 Kabila la Nafutali, Pedaheli mwana wa Amihudi.

29 Hawa ndio watu ambao Yawe aliwaamuru wawagawanyie watu Waisraeli inchi ya Kanana kuwa mali yao.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ