Hesabu 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maji ya Meriba ( Kut 17.1-7 ) 1 Waisraeli wote wakafika katika jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza, wakapiga kambi yao huko Kadesi. Wakiwa huko, Miriamu akakufa na kuzikwa. 2 Pahali pale walipopiga kambi hapakukuwa maji. Kwa hiyo watu wote pamoja wakakusanyika mbele ya Musa na Haruni. 3 Wakagombanisha Musa wakisema: Afazali tungekufa pamoja na wandugu zetu mbele ya hema la Yawe! 4 Kwa nini mulituleta sisi watu wa Yawe huku katika jangwa? Mulituleta kusudi tukufe pamoja na mifugo yetu? 5 Kwa nini mulitutoa Misri na kutuleta pahali hapa pabaya hivi? Hapa si pahali pa ngano, tini, zabibu wala makomamanga. Hata maji ya kunywa hakuna! 6 Hapo, Musa na Haruni wakaondoka kwenye mukutano wa watu, wakaenda kusimama kwenye mulango wa hema la mukutano, wakainama uso mpaka chini. Basi, utukufu wa Yawe ukawatokea, 7 naye Yawe akamwambia Musa: 8 Twaa ile fimbo yako, kisha wewe na ndugu yako Haruni mukusanye watu wote pamoja. Halafu, mbele ya macho yao, uambie jiwe linalokuwa mbele ya macho yao litoe maji yake. Utawatoshea maji ndani ya jiwe watu wote na mifugo yao waweze kunywa. 9 Musa akaenda kuitwaa ile fimbo mbele ya Yawe kama vile alivyoamriwa. 10 Kisha Musa na Haruni wakawakusanya watu wote pamoja mbele ya jiwe, naye Musa akawaambia: Musikilize sasa, enyi waasi; tuwatokezee maji kutoka katika jiwe hili? 11 Kisha Musa akainua mukono wake, akapiga lile jiwe mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika kwa wingi, watu wakakunywa pamoja na mifugo yao. 12 Lakini Yawe akamwambia Musa na Haruni: Kwa sababu ninyi hamukuniamini mimi, wala kuniheshimu mbele ya macho ya Waisraeli, basi kwa sababu hiyo hamutaingiza watu hawa katika ile inchi niliyowapa. 13 Hayo ni maji ya Meriba, ni kusema ya “Magombano”, pahali ambapo Waisraeli walimugombanisha Yawe, naye akajionyesha kwa utakatifu kati yao. Mufalme wa Edomu anawazuia Waisraeli kupita 14 Musa akatuma wajumbe kutoka Kadesi kwa mufalme wa Edomu akamwambia: Ndugu yako Israeli anasema hivi: Wewe unajua taabu zote tulizozipata. 15 Jinsi babu zetu walivyokwenda Misri, ambako tuliishi kwa muda murefu na jinsi Wamisri walivyowatesa babu zetu, wakatutesa na sisi vilevile. 16 Tukamulilia Yawe, naye akasikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri. Sasa tuko hapa Kadesi, muji unaopakana na inchi yako. 17 Tafazali uturuhusu tupite katika inchi yako. Hatutakanyaga mashamba yenu, wala yale ya mizabibu; wala hatutakunywa maji ya visima vyenu. Tutafuata barabara kubwa ya mufalme na kwenda moja kwa moja bila kugeuka kuume au kushoto, mpaka tutakapotoka katika inchi yako. 18 Lakini mufalme wa Edomu akamujibu: Hapana! Hautapita katika inchi yangu, kama ukipita nitatoka na kukushambulia kwa upanga. 19 Waisraeli wakamwambia: Sisi tutafuata njia kubwa; kama sisi na mifugo yetu tukikunywa maji yenu, tutalipa. Tunachoomba tafazali uturuhusu tu, tupite kwa miguu wala hatutaki neno lolote lingine. 20 Lakini mufalme wa Edomu akajibu: Hatutawaruhusu. Mara moja, Waedomu wenye nguvu wakatoka kupigana nao. 21 Basi, Waedomu wakakataa kuwapa Waisraeli ruhusa kwa kupita katika mipaka yao. Waisraeli wakageuka na kushika njia ingine. Kifo cha Haruni 22 Waisraeli wote wakasafiri kutoka Kadesi, wakafika kwenye mulima Hori. 23 Basi, Yawe akamwambia Musa na Haruni huko kwenye mulima Hori, kwenye mpaka wa inchi ya Edomu: 24 Haruni atakufa; hataingia katika inchi ambayo nimewapa Waisraeli kwa sababu ninyi wawili muliasi amri yangu kule Meriba. 25 Umutwae Haruni na mwana wake Eleazari, uwalete juu ya mulima Hori. 26 Kisha, umuvue Haruni nguo yake, umuvalishe mwana wake Eleazari. Haruni atakufa akiwa huko kwenye mulima. 27 Musa akafanya kama vile alivyoamriwa na Yawe. Wote watatu wakapanda juu ya mulima mbele ya watu wote wengine. 28 Kisha Musa akamuvua Haruni nguo zake, akamuvalisha mwana wake, Eleazari. Naye Haruni akakufa palepale kwenye mulima. Kisha Musa na Eleazari wakateremuka chini. 29 Waisraeli walipoona kwamba Haruni amekufa, wakafanya kilio cha siku makumi tatu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo