Amosi 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu kwa kuichoma mifupa yake kwa moto kwa kujitengenezea chokaa! 2 Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Moabu, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za muji wa Kerioti. Waaskari watakapolalamika kwa sauti zao na kupiga baragumu, watu wa Moabu watakufa katika makelele hayo ya vita. 3 Nitamwua mutawala wa Moabu, pamoja na waongozi wote wa inchi hiyo. –Ni Yawe anayesema hivyo. Yuda 4 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamezarau sheria zangu, wala hawakufuata masharti yangu. Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata. 5 Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema. Hukumu ya Mungu juu ya Israeli 6 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao; na kuwauzisha wakosefu wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa. 7 Wanagandamiza wazaifu, na kuwabagua wamasikini wasipate haki zao. Mutoto na baba yake wanalala na binti mujakazi mumoja, hivyo wanalichafua jina langu takatifu. 8 Juu ya kila mazabahu, watu wanalalia nguo walizozitwaa kwa masikini kama rehani ya madeni yao; na katika nyumba ya Mungu wao, wanakunywa divai waliyotwaa kwa wenye kuwa na madeni yao. 9 Hata hivyo, enyi watu wangu, kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori ambao walikuwa wakubwa kama mierezi, wenye nguvu kama miti ya mialo. Niliwaangamiza, matawi na mizizi. 10 Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu. 11 Nilichagua manabii kati ya wana wenu, na wengine kati ya vijana wenu kuwa wanaziri. Enyi Waisraeli, haya ninayosema si ya kweli? –Ni ujumbe wa Yawe.– 12 Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai, na kuwaamuru manabii wasitoe unabii. 13 Sasa basi, nitawagandamizia chini, kama gari lililojaa ngano. 14 Hata wale wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kutoroka; wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na waaskari watashindwa kuyaokoa maisha yao. 15 Wapiga upinde katika vita hawataweza kusimama na nguvu; wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kujiokoa, wala waaskari wapanda-farasi hawatayaokoa maisha yao. 16 Siku hiyo, hata waaskari hodari sana watakimbia mbio bila chochote. –Ni ujumbe wa Yawe. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo