Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

2 Watesalonika 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mutuombee

1 Kwa mwisho wandugu, mutuombee, kusudi neno la Bwana lisambae upesi na kutukuzwa, kama vile inavyokuwa kwenu.

2 Vilevile mumwombe Mungu kusudi atuopoe toka mikono ya watu wabaya na waovu. Kwa maana si watu wote wanaokubali kuamini Habari Njema.

3 Lakini Bwana ni mwaminifu, atawaimarisha na kuwakinga na yule Mwovu.

4 Bwana anatupatia tumaini kwa ajili yenu kwamba munafanya na mutaendelea kufanya yale tunayowaagiza.

5 Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Inafaa kutumika kazi

6 Wandugu, tunawaagiza katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba mujitenge na wandugu wote wanaokuwa wavivu na wasiofuata mafundisho tuliyowapa.

7 Munajua vizuri ninyi wenyewe namna munavyopaswa kuiga mufano wetu. Kwa maana sisi hatukukuwa wavivu wakati tulipoishi pamoja nanyi.

8 Sisi hatukukula chakula cha mutu kwa bure, lakini tulitumika na kuchoka sana. Tulitumika muchana na usiku kusudi tusilemee hata mutu mumoja kati yenu.

9 Tulifanya vile si kwa sababu hatukukuwa na haki ya kupokea musaada wenu, lakini kwa sababu tulitaka sisi wenyewe kuwa kwenu mufano wa kuiga.

10 Kwa maana, wakati tulipokuwa kwenu, tulikuwa tunawaagiza hivi: “Mutu yeyote asiyetaka kutumika, na hapaswi kula vilevile.”

11 Tunasema hivi kwa sababu tumepata habari kwamba wamoja kati yenu ni wavivu; hawatumiki, isipokuwa tu kujiingiza katika maneno ya wengine.

12 Tunawaagiza watu wale na kuwaonya kwa jina la Bwana Yesu Kristo kwamba watumike katika utulivu kwa kujitoshelea wenyewe katika maisha yao.

13 Lakini ninyi, wandugu, musichoke kutenda mema.

14 Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.

15 Musimuhesabu kama vile adui, lakini mumwonye kama vile ndugu.


Baraka na salamu

16 Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.

17 Hii ni salamu ninayoiandika kwa mukono wangu mimi Paulo mwenyewe. Hii ndiyo sahihi yangu katika kila barua yangu, na mwandiko wangu.

18 Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Yesu Kristo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ