Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

2 Watesalonika 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Siku ya kurudia kwa Bwana

1 Sasa tunawaandikia juu ya mambo yanayoelekea kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo na namna sisi tutakavyokusanyika mbele yake. Wandugu, tunawasihi sana,

2 musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.

3 Musikubali kudanganywa na mutu yeyote kwa namna yoyote. Kwa maana Siku ile haitatimia mpaka kwanza ule uasi mukubwa utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa.

4 Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.

5 Hamukumbuki kwamba niliwaambia maneno haya wakati nilipokuwa pamoja nanyi?

6 Lakini munajua kitu kinachozuiza mambo haya kutokea sasa. Kwa hivi yule Mwovu atatokea kwa wakati wake uliopangwa.

7 Hata hivi yule Mwovu anatenda kazi zake kwa siri; lakini yule anayezuiza ataendelea hata atakapoondoshwa.

8 Halafu, yule Mwovu atatokea, lakini Bwana Yesu atakapotokea atamwua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa nguvu za kumetameta kwake.

9 Mwovu atakuja na uwezo wa Shetani na kufanya miujiza ya kila namna, vitambulisho na maajabu ya uongo.

10 Atatumia ubaya wa kila namna kwa kuwadanganya wale wanaopotea kwa sababu hawakupenda kukubali na kupenda mambo ya kweli yaliyoweza kuwaokoa.

11 Kwa sababu hii Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu wapate kuamini mambo ya uongo.

12 Kwa hivi wale wote wasioamini maneno ya ukweli, waliofurahia mambo mabaya watahukumiwa.


Kusimama imara katika imani

13 Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.

14 Mungu amewaalika kuwa vile kwa njia ya Habari Njema tuliyowatangazia, kusudi mupate kushiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.

15 Basi wandugu, musimame imara na mushike mafundisho yetu tuliyowatolea, ikiwa kwa mahubiri au kwa barua yetu.

16 Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,

17 awafariji na kuwaimarisha katika matendo na maneno yote mema.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ