Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

2 Wafalme 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mufalme Yoasi wa Yuda
( 2 Sik 24.1-16 )

1 Yoasi alianza kutawala inchi ya Yuda akiwa na umri wa miaka saba.

2 Katika mwaka wa saba wa utawala ya mufalme Yehu wa Israeli, Yoasi alianza kutawala Yuda kule Yerusalema, naye akatawala kwa muda wa miaka makumi ine akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Sibia wa Beri-Seba.

3 Wakati wa maisha yake yote alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kwa sababu kuhani Yehoyada alikuwa akimufundisha.

4 Hata hivyo, nafasi za kuabudu miungu kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kule.

5-6 Yoasi akaita makuhani na kuwaamuru, akisema: “Kila kuhani apokee feza yote inayotolewa katika nyumba ya Yawe: ni kusema malipo ya kodi za hekalu na matoleo ya mapenzi. Azipokee kutoka kwa yeyote anayemufahamu kwa kutengeneza nyumba popote panapohitajika.”

7 Lakini hata nyuma ya miaka makumi mbili na mitatu ya utawala wa Yoasi, makuhani walikuwa bado hawajatengeneza hata mabomoko ya nyumba.

8 Kwa hiyo mufalme Yoasi alimwita kuhani Yehoyada na makuhani wengine na kuwauliza: “Mbona hamujatengeneza nyumba? Basi, sasa hamutapokea tena feza kutoka kwa wengine lakini zitaletwa kusudi nyumba itengenezwe.”

9 Makuhani wakakubali wasipokee feza tena kutoka kwa watu. Vilevile hawakukuwa na madaraka ya kutengeneza nyumba ya Yawe.

10 Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.

11 Kila mara walipoona kwamba kuna feza nyingi ndani ya sanduku, mwandishi wa mufalme na Kuhani Mukubwa waliingia na kupima feza yote iliyopatikana katika nyumba ya Yawe.

12 Halafu kisha kuzipima walizitoa kwa wafanyakazi waliosimamia nyumba ya Yawe, nao wakazilipa kwa waseremala na wenye kujenga waliotengeneza nyumba ya Yawe,

13 kwa wajengaji na wenye kuchonga mawe, na zikatumiwa kwa kununua mbao na mawe yaliyochongwa kwa kutengeneza nyumba ya Yawe na kutimiza mahitaji mengine yote ya kazi ya kutengeneza nyumba.

14 Lakini feza zake hazikutumiwa kwa kulipa kazi za kutengeneza mabeseni ya feza, makasi ya kukata tambi za mishumaa, mabakuli, baragumu, wala kwa vyombo vingine vyovyote vya zahabu au vya feza.

15 Zote zilitumiwa kwa kuwalipa wafanyakazi waliozitumia kwa kutengeneza nyumba ya Yawe.

16 Wafanyakazi waliosimamia kazi hii walikuwa waaminifu kabisa. Kwa hiyo hakukuwa lazima ya kuwaomba watoe hesabu ya matumizi ya feza.

17 Feza zilizotolewa kwa sadaka za malipo kwa ajili ya kosa na kwa sadaka za usamehe wa zambi hazikuingizwa katika nyumba ya Yawe. Hizo zilikuwa ni mali ya makuhani.

18 Wakati huo Hazaeli mufalme wa Aramu akaushambulia muji wa Gati na kuuteka. Lakini Hazaeli alipoelekea Yerusalema kusudi aushambulie,

19 Yoasi mufalme wa Yuda alitwaa sadaka zote zilizotakaswa na babu zake wafalme wa Yuda: Yosafati, Yehoramu na Ahazia, na kuongeza zile zake, pamoja na zahabu yote iliyokuwa katika hazina ya nyumba ya Yawe na katika nyumba ya kifalme, akazituma kwa Hazaeli mufalme wa Aramu. Naye Hazaeli akatoka Yerusalema.

20 Mambo mengine ya Yoasi na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.

21 Wakubwa wa serikali yake wakamwasi, wakamwuia katika uwanja wa Milo kwenye barabara inayoelekea Sila.

22 Waliomwua ni Yozakari mwana wa Simeati na Yozabadi mwana wa Someri watumishi wake. Halafu wakamuzika katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi. Naye Amazia mwana wake akatawala kwa pahali pake.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ