Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

1 Watesalonika 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kwa mwisho hatukuweza kuvumilia tena. Basi, tuliona vema kubaki Atene peke yetu

2 na kumutuma ndugu yetu Timoteo, anayemutumikia Mungu pamoja nasi katika kazi ya kutangaza Habari Njema ya Kristo. Tulimutuma kwenu apate kuwatia nguvu na kuwafariji katika imani yenu,

3 kusudi hata mumoja wenu asitikiswe na mateso haya tunayopata. Ninyi wenyewe munajua vema kwamba mateso kama hayo yalipaswa kututokea.

4 Kwa maana wakati tulipokuwa pamoja nanyi, tulikuwa tumekwisha kuwaambia mbele ya wakati kwamba tutapata mateso. Na ni vile ilivyotutokea kama munavyojua.

5 Ni kwa sababu hiyo, nilipoona kwamba siwezi kuendelea kungojea, nilimutuma Timoteo kusudi nipate kujua habari ya imani yenu. Niliogopa kwamba labda yule mushawishi Shetani amejaribu kuwaangusha ninyi na kwamba kazi yote tuliyofanya kwenu imepotea bure.

6 Lakini sasa Timoteo amefika kwetu, akirudia toka kule kwenu. Ametuletea habari nzuri juu ya imani yenu na upendo wenu. Ametuelezea kwamba munatukumbuka vizuri siku zote, na kwamba muko na hamu sana ya kutuona, kama vile sisi nasi tunavyokuwa na hamu ya kuwaona.

7 Kwa hiyo wandugu, katika taabu na mateso tunayopata, tumefarijiwa nanyi kwa kusikia habari za imani yenu.

8 Kwa maana sasa tunaweza kupumua kwa kuona munasimama imara katika kuungana kwenu na Bwana.

9 Sijui namna gani tunavyoweza kumushukuru Mungu kwa ajili yenu kwa sababu ya furaha yote tunayokuwa nayo mbele yake kwa ajili yenu.

10 Usiku na muchana tunamwomba Mungu kwa bidii sana kusudi atupatie njia ya kuweza kuwaona tena na kuwaongezea kile munachokosewa katika imani yenu.

11 Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, watufungulie njia tupate kufika kwenu.

12 Na Bwana awaongezee na kuwazidishia upendo munaokuwa nao ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tunavyowapenda ninyi.

13 Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ