Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

1 Watesalonika 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kazi Paulo aliyotimiza kule Tesalonika

1 Wandugu, munajua ninyi wenyewe kwamba safari yetu kwenu haikukuwa bure.

2 Kama vile munavyojua, mbele ya kufika kwenu tuliteswa na kutukaniwa kwanza katika muji Filipi. Lakini ingawa tulipata vizuizo vingi, Mungu alitupatia uhodari wa kuwapasha ninyi Habari yake Njema.

3 Mahubiri yetu si ya uongo, wala yenye nia mbaya wala ya udanganyifu.

4 Lakini siku zote tunasema vile Mungu anavyotaka, kwa maana yeye aliamua kwamba tunastahili, akatupatia kazi ya kuhubiri Habari Njema yake. Sisi hatutafuti kuwapendeza watu, lakini tunataka kupendeza Mungu, anayejua siri za mioyo yetu.

5 Kama vile munavyojua, hata siku moja hatukutumia masemi ya kujipendekeza kwa watu wala hatukutamani kupata mali kwa uficho; Mungu ni mushuhuda wetu.

6 Hatukutafuta sifa ya watu wala yenu, wala ya mutu mwingine yeyote,

7 ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.

8 Sisi tunawapenda sana hata tumekuwa tayari, si kuwatolea Habari Njema ya Mungu tu, lakini kutoa maisha yetu kwa ajili yenu vilevile. Ni vile kwa sababu ninyi mumekuwa kweli wapendwa wetu.

9 Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.

10 Ninyi ni washuhuda wetu, na Mungu vilevile anashuhudia kwamba tulipokaa kati yenu ninyi waamini, tuliishi katika utakatifu na haki, na bila kosa.

11 Munajua vizuri kwamba tulimutendea kila mumoja wenu kama vile baba anavyowatendea watoto wake mwenyewe.

12 Sisi tuliwaonya, tuliwafariji na kuwasihi sana muishi sawa inavyomupendeza Mungu, anayewaalika kushiriki naye katika ufalme na utukufu wake.

13 Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.

14 Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.

15 Ndio wale waliomwua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa sisi vilevile. Wao hawamupendezi Mungu, nao ni waadui za watu wote!

16 Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Paulo anatamani kuwaona Watesalonika

17 Wandugu, sisi kwa ngambo yetu, tuliachana nanyi kwa muda kimwili, lakini si kiroho. Nyuma ya pale tulifanya bidii sana kusudi tuwafikie.

18 Tulitaka kuja kule kwenu, zaidi sana mimi Paulo nilijaribu kufunga safari mara moja au mara mbili hivi, lakini Shetani alituzuiza.

19 Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.

20 Kweli, ni kwa ajili yenu sisi tunajivuna na kufurahi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ