Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -

1 Samweli 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Saulo anawashinda Waamoni

1 Mufalme Nahasi wa Waamoni, alikwenda na kuushambulia muji wa Yabesi-Gileadi. Wakaaji wa muji wa Yabesi-Gileadi wakamwambia Nahasi: “Fanya mapatano nasi, nasi tutakutumikia.”

2 Lakini akawaambia: “Nitafanya mapatano nanyi kwa shurti hii moja: nitamwongoa kila mumoja wenu jicho lake la kuume. Hivyo nitawapatisha Waisraeli wote haya.”

3 Wazee wa Yabesi wakamwambia: “Utupatie muda wa siku saba kusudi tuwatume wajumbe katika inchi yote ya Waisraeli. Kama hakuna mutu yeyote wa kutuokoa, tutajitoa sisi wenyewe kwako.”

4 Wale wajumbe walipofika katika muji wa Gibea, ambako Saulo alikoishi, wakaeleza habari hizo na watu wote wakaanza kulia kwa sauti.

5 Sasa, Saulo alikuwa anatoka kwenye shamba akiwa na ngombe dume wake, akauliza: “Watu wana nini? Kwa nini wanalia?” Wakamwambia habari wajumbe waliyoleta kutoka Yabesi.

6 Mara moja, Saulo aliposikia maneno hayo, roho wa Mungu akamufikia kwa nguvu, naye akawaka hasira kali.

7 Akatwaa ngombe dume wawili, akawakatakata vipande, akatuma wajumbe wapitishe vipande hivyo katika mipaka yote ya Waisraeli wakisema: “Mutu yeyote ambaye hatamufuata Saulo na Samweli katika vita, ngombe dume wake watafanyiwa hivyo.” Waisraeli waliingiwa na hofu juu ya kile ambacho Yawe angeweza kufanya. Kwa hiyo, wote walitoka pamoja.

8 Saulo alipowapanga Waisraeli kule Bezeki akakuwa na watu elfu mia tatu kutoka inchi ya Israeli na elfu makumi tatu kutoka inchi ya Yuda.

9 Wakawaambia wale wajumbe waliorudi kutoka Yabesi: “Muwaambie wakaaji wa Yabesi-Gileadi hivi: kesho, wakati jua linapokuwa kali, mutakuwa mumekombolewa.” Watu wa Yabesi walipopata habari hizo walifurahi sana.

10 Hivyo, wakamuchekelea Nahasi wakimwambia: “Kesho tutajitoa wenyewe kwako, nawe utatutendea sawa unavyotaka.”

11 Kesho yake, Saulo aliwagawanya watu katika vikundi vitatu. Wakati wa zamu ya asubui, wakaingia kwenye kambi ya adui, na kuwashambulia Waamoni. Kufikia saa sita za muchana waadui wengi walikuwa wameangamizwa. Wale waliobaki walitawanyika ovyo, hata hakukuwa kikundi chochote kati yao hata cha watu wawili tu pamoja.

12 Halafu Waisraeli wakamwambia Samweli: “Wako wapi wale watu waliosema Saulo asikuwe mufalme juu yetu? Mutuletee watu hao, nasi tutawaua.”

13 Lakini Saulo akawaambia: “Hakuna mutu yeyote atakayeuawa leo, kwa sababu katika siku hii, Yawe ameikomboa Israeli.”

14 Samweli akawaambia: “Twende wote Gilgali na kwa mara ingine tutamutangaza Saulo kuwa mufalme.”

15 Watu wote wakaenda Gilgali, na walipofika kule, wakamusimika Saulo kuwa mufalme mbele ya Yawe. Wakamutolea Yawe sadaka za amani pale. Na Saulo pamoja na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:



ကြော်ငြာတွေ