Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 3:13
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


Utalala bila kuogopeshwa na mutu; watu wengi watakuomba musaada.


watu wasiotenda uovu hata kidogo, lakini wanafuata siku zote njia zake.


Uniokoe, ee Yawe, kutoka watu wadanganyifu na waongo.


Enyi watu wadanganyifu, mutapewa kitu gani? Mutaazibiwa namna gani?


Ananipumzisha kwenye majani mabichi; ananiongoza kando ya maji matulivu,


Miji inayokuwa chini yake imeachwa matongo milele. Itakuwa makao ya makundi ya nyama, wala hakuna mutu atakayewatisha.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Bonde la Saroni litakuwa nafasi ya kukulishia nyama, bonde la Akori litakuwa mapumziko ya ngombe kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.


Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea. –Ni ujumbe wa Yawe.


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Watakapokuwa wanaishi kwa usalama katika inchi yao, bila kutishwa, watasahau haya yao na uasi walionitendea.


Nitawapa amani katika inchi hata muweze kulala bila kuogopeshwa na chochote. Nitaondoa nyama wakali katika inchi na inchi yenu haitapatwa na vita.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


Hivi ndivyo munavyopaswa kufanya: Kila mumoja wenu amwambie mwenzake ukweli. Tribinali zenu zitoe siku zote hukumu za haki zinazoleta amani.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Musiambiane uongo ninyi kwa ninyi, kwa maana mumeondoa utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake


Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.


Tunajua kwamba kila mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa maana Mwana wa Mungu anamulinda, wala yule Mwovu hawezi kumugusa.


Wao hawakusema uongo hata mara moja; wako bila kosa.


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ