Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 3:11
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi. Ee Yawe, sina moyo wa majivuno; wala macho yangu si ya kiburi. Sijishugulishi na mambo makubwa, yale yanayokuwa ya ajabu sana kwangu.


Ninatega sikio, nisikilize mezali, ninafafanua kitendawili kwa muziki wa zeze.


Usiwaue mara moja, watu wangu wasisahau; uwasambazesambaze kwa nguvu yako, uwaporomoshe chini. Ee Bwana, wewe ndiwe ngao yetu!


Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari.


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Kila mutu atafezeheshwa, na wenye kiburi wote watapatishwa haya.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Kwa vile mulipata haya mara mbili, watu wakaona kwamba mazarau ni majaliwa yenu, sasa mutapata sehemu mara mbili kuwa mali yenu, na furaha yenu itadumu milele.


Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.


Musitumainie maneno haya ya udanganyifu mukisema: Hili ni hekalu la Yawe, hekalu la Yawe, hakika hili ni hekalu la Yawe.


Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuwa na hasira kwa ajili ya muji wako Yerusalema, mulima wako mutakatifu. Watu wote wa inchi za jirani wanauzarau Yerusalema na watu wako, kwa sababu ya zambi zetu na maovu babu zetu waliyotenda.


Basi, nilipokuwa nikiomba, nikiitikia zambi zangu na zambi za watu wangu wa inchi ya Israeli, pamoja na kumusihi Yawe kwa ajili ya mulima wake mutakatifu,


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Wakakusanyika mbele ya Musa na Haruni, wakawaambia: Ninyi mumepitisha kipimo! Waisraeli wote pamoja ni watakatifu; kila mumoja ni mutakatifu. Yawe yuko pamoja nasi wote. Mbona sasa ninyi munajifanya wakubwa kushinda watu wengine wa Yawe?


Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


Sasa wewe unaitwa Muyuda, unategemea Sheria na kujivunia Mungu.


kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni nalo ni la kuangusha. Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”


Kwa kuwa imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: “Nimesimika jiwe kubwa la pembe katika Sayuni, jiwe lile ni la bei kali. Ni mimi niliyelichagua. Yule anayelitumainia hatapata haya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ