Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 2:9
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


Inua macho uangalie pande zote; watu wako wote wanakusanyika na kukufikia. Kama vile ninavyoishi, watu wako watakuwa kwako kama mapambo, utawafurahia kama vile bibi arusi anavyofanya na taji lake. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi– kweli adui anakuja kuwashambulia: ni hakika kama vile Tabori unavyokuwa mulima, kama vile mulima Karmeli unavyoonekana kutoka katika bahari.


Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;


Juu ya Waamoni, Yawe anasema hivi: Israeli hana watoto? Hana warizi? Mbona basi mungu Milkomu ametwaa Gadi na watu wake wanafanya makao yao katika miji yake?


Kama vile Sodoma na Gomora na miji jirani yake ilivyoangamizwa, hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi Edomu wala kufanya mashauri humo. –Ni Yawe anayesema.–


Muji wa Hazori utakuwa makao ya mbweha, utakuwa jangwa siku zote; hakuna mutu atakayekaa humo, wala atakayeishi humo.


Kama vile mimi Yawe nilivyoiangamiza miji ya Sodoma na Gomora na miji ya jirani, vilevile hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi humo. Kweli, hakuna mutu yeyote atakeyekaa huko. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu kwa kuichoma mifupa yake kwa moto kwa kujitengenezea chokaa!


Makundi ya nyama wa kufugwa watalala ndani yake, vilevile kila nyama wa pori. Tai, nyangenyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake, bundi watalia kwenye madirisha yake, vibombobombo watalia kwenye vizingiti, maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.


Lakini kwa kweli, kama vile ninavyoishi na kama vile dunia itakavyojaa utukufu wa Yawe,


Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Bwana anasema: Kama vile ninavyoishi, kila mutu atapiga magoti mbele yangu, na kila mutu ataitikia kwamba mimi ni Mungu.”


Wataona kwamba imejaa kiberiti na chumvi, imechomwa na kuwa tupu, haikupandwa mbegu na haioti chochote. Ni kama vile ilivyokuwa wakati Yawe alipoangamiza Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu, kwa hasira yake kali.


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ