Watu wa Yuda wanasema hivi: Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, tunajua jinsi alivyojivuna sana; tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake; lakini majivuno yake hayo ni bure.
Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.
Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;
Juu ya Waamoni, Yawe anasema hivi: Israeli hana watoto? Hana warizi? Mbona basi mungu Milkomu ametwaa Gadi na watu wake wanafanya makao yao katika miji yake?
Lakini watu wa Yerusalema watauzania kuwa ni utabiri wa uongo kwa sababu ya mapatano waliyofanya. Hata hivyo unabii huu utawakumbusha uovu wao na kusababisha kukamatwa kwao.
Wewe utajua kwamba mimi mwenyewe Yawe nimeyasikia matusi yote uliyoyatoa juu ya milima ya Waisraeli, ukisema: Milima ya Israeli imefanywa kuwa jangwa! Imetolewa kusudi tupate kuinyanganya!
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu kwa kuichoma mifupa yake kwa moto kwa kujitengenezea chokaa!