Zefania 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20027 Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Watu watanunua mashamba kwa feza, watazitia sahihi barua zake za ununuzi, watazipiga muhuri, na kuweka washuhuda katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema, katika miji ya Yuda, katika miji ya inchi ya milima, katika miji ya Shefela, na katika miji ya jangwa la Negebu. Maana nitawastawisha tena. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.