Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 2:5
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Musishangilie, enyi Wafilistini wote, kwamba Asuria, fimbo iliyowapiga, imevunjika; maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu, na nyoka mwenye sumu atazaa nyoka mukubwa mwenye kuruka.


Wazaliwa wa kwanza wa wazaifu watashiba, na wakosefu watakaa kwa usalama. Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa; na yeyote kati yenu atakayebaki nitamwua.


Lakini utaweza kutulia namna gani, ikiwa ni Yawe ameupa kazi? Ameuamuru ushambulie muji wa Askeloni na watu wanaoishi kandokando ya bahari.


basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi: Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli:


Mulie, enyi wakaaji wa Makitesi! Wachuuzi wote wameangamia, wote wanaopima feza wameteketezwa.


Yawe anasema: Nimeyateketeza kabisa mataifa; kuta zao za kujikinga ni mabomoko. Barabara zao nimeziharibu, na hakuna anayepita ndani yake. Miji yao imekuwa mitupu, bila watu, na bila wakaaji.


Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea.


Basi hao wakubwa wakatafuta kumukamata Yesu, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao. Lakini kwa sababu waliogopa kundi la watu, wakamwacha ajiendee.


Sehemu hizo ni: inchi yote ya Wafilistini na inchi yote ya Wagesuri,


ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,


Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ